Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 8 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 69 2017-04-18

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. DEO F. NGALAWA Aliuliza:-
Shirika la Posta Tanzania lilitumia fedha zake kuwalipa Wastaafu wa lililokuwa Shirika la Posta na Simu la Afrika Mashariki:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kulirejeshea Shirika hilo fedha hizo ili kulinusuru?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO Alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deo Francis Ngalawa, Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli Shirika la Posta Tanzania lilitumia fedha zake kuwalipa wastaafu wa lililokuwa Shirika la Posta na Simu la Afrika Mashariki na kuwasilisha madai Serikalini ili lipate kurejeshewa fedha zake. Hadi sasa Shirika limelipa shilingi bilioni 5.9 na Serikali imesharejesha shilingi bilioni 2.7 kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Spika, Novemba, 2016 Serikali ilirejesha Shilingi milioni 700; Desemba, 2016 Shilingi 1,000,000,000; na Januari, 2017, Serikali ilirejesha Shilingi 1,000,000,000. Aidha, Serikali itaendelea kurejesha kiasi kilichobaki cha Shilingi 3,200,000,000 kwa kadri fedha zitakavyopatikana.
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Msajili wa Hazina inaendelea na jukumu la kuwalipa pensheni ya kila mwezi wastaafu wa lililokuwa Shirika la Posta na Simu la Afrika Mashariki wapatao 292.