Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 5 2016-04-19

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. KABWE Z. R. ZITTO) aliuliza:-
Je, ni lini Mradi wa kuzalisha umeme wa Malagarasi utaanza?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kabwe Ruyagwa Zitto, Mbunge wa Kigoma Mjini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, baada ya tafiti za kimazingira kuonesha kuwa utekelezaji wa miradi wa kuzalisha umeme katika Mto Malagarasi katika maeneo ya Igamba Na. III ungekuwa na athari za kumazingira, Serikali itafute eneo lingine. Eneo la Igamba Na. III, lilipatikana na Mkandarasi Mshauri ESBI alianza kazi ya upembuzi yakinifu mwezi Juni, 2010 kupitia ufadhili wa Mfuko wa Changamoto za Milenia (MCC I). Upembuzi yakinifu na usanifu wa awali (preliminary design) ulikamilika mwaka 2012 na kubainika kuwa maporomoko ya sehemu hiyo yana uwezo wa kuzalisha MW 44.8 na Mkandarasi Mshauri alipewa kazi ya kufanya upembuzi yakinifu na utekelezaji wa miradi kufanywa na Mfadhili mwingine.
Mheshimiwa Spika, hivi sasa TANESCO inaendelea na taratibu za kumpatia Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kufanya usanifu wa kina yaani (detail design) na kutengeneza nyaraka za zabuni (tender document) zitakazotumika kumpata mkandarasi wa ujenzi wa kazi hiyo. Mradi huu unakusudiwa kutekelezwa kwa njia ya EPC (Uhandisi, Manunuzi pamoja na Ujenzi).
Mheshimiwa Spika, taratibu za kumpata Mtaalam Mshauri zitakamilika mwezi Juni, 2016, kazi ya usanifu wa kina pamoja na taratibu za kumpata mkandarasi wa ujenzi itachukua miezi sita. Mkandarasi atakayepatikana ataanza kazi Februari, 2017 na utekelezaji wa mradi utachukua miaka mitatu, fedha zitakazotengwa katika mwaka wa fedha 2016/2017 kwa utekelezaji wa mradi huu ni shilingi bilioni tano.