Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 59 2017-04-13

Name

Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY F. OWENYA aliuliza:-
Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imekuwa na tatizo la kukatika umeme mara kwa mara.
(a) Je, ni sababu zipi zinazosababisha hali hiyo?
(b) Je, ni lini tatizo hili litakwisha?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lucy Fidelis Owenya, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kilimanjaro ni miongoni mwa mikoa inayofaidika na utekelezaji hali ya utekelezaji wa miradi ya TEDAP. Mradi huu unafadhiliwa na Benki ya Dunia na unalenga kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme nchini. Kazi za mradi huu kwa Mkoa wa Kilimanjaro
zinajumuisha kuongeza uwezo wa vituo viwili vya kupoza umeme vya Trade School kutoka MVA 5 hadi MVA 15. Pia kuboresha miundombinu hiyo katika maeneo ya Boma Mbuzi kutoka MVA 10 hadi MVA 15. Hali kadhalika kubadilisha waya katika njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 kutoka milimita 100 hadi milimita 150. Vilevile kuongeza uwezo wa kusafirisha umeme muhimu na bora.
Mheshimiwa Spika, mradi huu ulianza kutekelezwa mwezi Januari, 2014 na umekamilika kwa asilimia 95 ambapo sasa kilometa 50.95 kati ya kilometa 54.63 zimeshajengwa na waya zimeshaunganishwa.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha utekelezaji wa mradi huu kumekuwa na ulazima wa kuzia umeme katika baadhi ya maeneo ili kupisha marekebisho maalum na kwa usalama zaidi. Zoezi hili limekuwa likifanyika kwa kutoa taarifa katika vyombo mbalimbali vya habari. Tatizo la
kukatikakatika kwa umeme katika maeneo ya Halmashauri ya Mji wa Moshi litaisha mara baada ya shughuli za Mradi huu kukamilika mwezi Mei, 2017.