Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 49 2017-04-12

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Wananchi wa Mtaa wa Katoma na Magema katika Kata za Mtakuja na Kalangalula kwa muda mrefu wamezuiwa kuendeleza ardhi zao kwa sababu Mgodi wa GGM ulipima na kuweka vigingi vya mpaka ndani ya makazi yao.
Je, ni lini mgodi huo utawalipa fidia ili kupisha shughuli za mgodi huo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Madini ya mwaka 2010 huwataka wamiliki wa leseni za uchimbaji wa madini kuzingatia umbali uliowekwa kisheria kutoka sehemu ambako shughuli nyingine za kijamii zinaendelea. Kwa kuzingatia sheria hiyo, mgodi hulazimika kuwalipa fidia na kuhamisha wananchi wanaoishi ndani ya umbali wa mita 200 kutoka katika shughuli za uchimbaji ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea kutokana na uchimbaji huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mgodi wa GGM mwaka 2007, 2010, 2013 na 2014 ulilipa fidia ya jumla ya shilingi bilioni 9.67 kwa wananchi 733 wanaoishi ndani ya mita 570 katika maeneo ya Katoma na Nyamalembo. Hata hivyo, kwa kuwa mgodi haujaanza kutumia eneo hilo kwa shughuli za uchimbaji, baadhi ya wananchi waliopata fidia pamoja na wengine wapya, wamejenga tena katika maeneo hayo kwa ajili ya kudai fidia nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa eneo la Magema, mgodi hauzuii wananchi kuendesha shughuli za kilimo na kuendesha shughuli za kimaisha kwa sababu eneo hilo halihitajiki na mgodi kwa sasa. Mgodi utalazimika kulipa fidia kwa kuzingatia sheria husika iwapo mgodi utahitaji kuendeleza eneo hilo.