Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 36 2017-04-11

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MHE. ANATROPIA L.
THEONEST aliluiza:-
Mkao Makuu ya Wilaya ya Kyerwa yamewekwa katika Kata ya Kyerwa.
Je, ni mchakato gani ulifanyika mpaka Kata ya Kyerwa kuwa Makao Makuu ya Wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA
SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili eneo liwe na makao makuu ya Wilaya lazima wananchi washirikishwe kupitia mikutano mikuu ya Vijiji na Halmashauri za Vijiji, Kamati za Maendeleo za Kata, Mabaraza ya Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya na Kamati ya Ushauri ya Mikoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uamuzi wa kuifanya Kata ya Kyerwa kuwa Makao Makuu ya Wilaya ya Kyerwa ulitolewa baada ya kupitishwa na Baraza la Madiwani katika kikao cha tarehe 30 hadi 31 Oktoba, 2012 na Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera katika kikao chake cha tarehe 15 Machi, 2013 hivyo uamuzi wa mwisho kuhusu eneo la Rubwera katika Kata ya Kyerwa kuwa Makao Makuu ya Wilaya Kyerwa ulizingatia mapendekezo ya vikao hivyo vya kisheria.