Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2000-2005 | Session 12 | Sitting 4 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Kilimo, Mifugo na Uvuvi | 29 | 2017-04-10 |
Name
Lucia Ursula Michael Mlowe
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:-
Kilimo cha viazi katika Mkoa wa Njombe kimekuwa ni ukombozi kwa wananchi wa mkoa huo. Zao hilo ni la biashara lakini wananchi wameanza kukata tamaa kutokana na kupanda kwa bei za pembejeo, pembejeo kutokufika kwa wakati na kukosa soko la uhakika:-
Je, Serikali ipo tayari kuwaunganisha wakulima hao na kuwa na chama chao kitakachoweza kupigania haki za wakulima hao?
Name
William Tate Olenasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucia Michael Mlowe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikihimiza makampuni na mawakala wanaosambaza pembejeo za kilimo kuwafikishia pembejeo wakulima kwa wakati kabla ya msimu wa kilimo kuanza. Kutokana na juhudi ya Serikali kwa kushirikiana na makampuni yanayosambaza pembejeo, imewezesha ufikishwaji wa pembejeo ikiwemo mbolea na mbegu bora kwa bei ya soko kwa wakulima kwa wakati. Aidha, changamoto ya kupanda bei ya pembejeo inafanyiwa kazi kwa kuondoa tozo mbalimbali ili kupunguza bei ya pembejeo na kuwezesha wakulima kumudu kununua na kutumia pembejeo hizo. Vilevile Serikali inakamilisha mchakato wa manunuzi ya pamoja (bulk procurement), uondoaji au kupunguza tozo mbalimbali na gharama za usafirishwaji katika mbolea ambao utasaidia kuongeza upatikanaji na kupunguza bei ya mbolea.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inaendelea kuhimiza uzalishaji wa mbegu za viazi kupitia vikundi katika ngazi ya mkulima. Kupitia utaratibu huu wakulima wengi watamudu kununua mbegu za viazi kwa bei nafuu kwa vile zinazalishwa ndani ya kijiji. Pia kupitia SAGCOT wakulima nane wamepata mafunzo ya kuzalisha mbegu za viazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ambazo zitauzwa ndani ya mkoa na hivyo kuchangia upatikanaji wa mbegu za viazi kwa wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ipo tayari kuwaunganisha wakulima wa zao la viazi kwa kutumia taasisi zake katika kuunda ushirika ambao utasaidia kuanzisha chama chao kulingana na taratibu za uanzishwaji wa vyama vya ushirika. Jukumu hili litatekelezwa kupitia tume ya ushirika kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Halmashauri husika katika Mkoa wa Njombe.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved