Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 3 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 23 2017-04-06

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA Aliuliza:-
Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) ni hifadhi ya kipekee hapa nchini, Afrika na dunia kwa ujumla; hifadhi hii ina vivutio vya kipekee pamoja na kuwa na matumizi mseto (multiple land use) ambapo wanyama na mifugo inachungwa pamoja; kutokana na upekee huo hifadhi hii imetambuliwa
na kuwekwa kwenye maajabu saba ya dunia chini ya Shirika la Uhifadhi Dunia (UNESCO).
Je, Serikali ina mpango gani endelevu wa kuhakikisha hadhi ya hifadhi hii inabaki kwenye ubora wake kwa ajili ya vizazi vya leo na vijavyo na pia kwa uchumi wa Taifa letu?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII Alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Magdalena Hamis Sakaya, Mbunge wa Kaliua, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa eneo la hifadhi la Ngorongoro ni muhimu na lina hadhi ya kipekee inayotokana na wingi na ubora wa vivutio vyake ambavyo vinatambulika Kitaifa na Kimataifa. Vivutio hivyo ni pamoja na matumizi mseto ya eneo, uwepo wa viumbe hai walioko hatarini
kutoweka duniani na umuhimu wa kihistoria uliothibitishwa na tafiti mbalimbali kuwa binadamu wa kwanza aliishi katika eneo hilo takriban miaka milioni 3.6 iliyopita. Aidha, kutokana na sifa hizo Shirika la Umoja wa Mataifa la UNESCO kupitia orodha yake ya maeneo ya urithi wa dunia (World Heritage Sites) imelipatia eneo hilo hadhi ya kimataifa, ambapo tangu mwaka 1979 limekuwa moja ya maeneo ya Urithi wa Dunia
kwa kigezi cha thamani ya maliasili iliyomo (The Integrity for natural value).
Mheshimiwa Spika, pamoja na sifa zilizotajwa hapo juu, kuanzia Februari, 2010 eneo hili limepewa hadhi nyingine kwa kigezo cha eneo la rasilimali mseto za maliasili, malikale na utamaduni yaani the mixed heritage value hivyo basi kwa kutambua upekee huo kwa Taifa, Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa eneo hili linabaki katika viwango bora vya uhifadhi kwa kuchukua hatua zifuatazo:-
(a) Kudhibiti ongezeko la idadi ya watu na mifugo ndani ya eneo la hifadhi, zoezi ambalo litaanza rasmi tarehe 12 Aprili, 2017 na kukamilika mwezi Juni, 2017. Aidha, wadau mbalimbali watashirikishwa katika zoezi hili ikiwemo mamlaka za Mkoa na mamlaka ya Wilaya, Taasisi ya Taifa ya Takwimu, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa na TAMISEMI.
(b) Kuendelea kuimarisha ulinzi wa wanyamapori na maeneo yote muhimu kwa shughuli za utalii kama vile crater na kutoruhusu shughuli za kibinadamu katika maeneo hayo.
(c) Kufanya mapitio ya sheria iliyoanzisha Mamlaka ya Hifadhi na kuiboresha ili iendane na hali halisi ya sasa.
Zoezi hili liko katika hatua za awali na linatarajiwa kukamilika katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018.