Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 68 2017-02-06

Name

Abdulaziz Mohamed Abood

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Mjini

Primary Question

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD aliuliza:-
Maeneo mengi katika Jimbo la Morogoro Mjini bado hawajapata nishati ya umeme kama vile Kata za Mindu, Lugala, Mkundi, Kiegea A na B, Kihonda, Mafisa, Tungi, Kingolwira na Kauzeni A.
Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo hili la muda mrefu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdul-Aziz Abood, Mbunge wa Morogoro Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Shirika la Umeme (TANESCO) inatekeleza miradi ya kufikisha miundombinu ya umeme maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na Morogoro Mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi unaoendelea katika Kata za Mindu, ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 8.973, ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti nne yenye urefu wa kilometa 35.4, lakini ufungaji wa transfoma saba pamoja na kuwaunganishia umeme wateja 834.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu utafikisha umeme kwenye maeneo ya Mindu, Kasanga na Madanganya ambapo ni transfoma nne zimefungwa tayari na baadhi ya wananchi pia wameshaunganishiwa umeme. Gharama za mradi ni shilingi bilioni 1.113. Unajumuisha Mindu -Lugala ambao unajumuisha ujenzi wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 8.9, ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa voti 400 yenye urefu wa kilometa 10.7 na ufungaji wa transfoma tatu. Hali kadhalika utaunganishwa umeme kwa wateja 206. Gharama za mradi huu ni milioni 106.784. Utekelezaji wa miradi hii utakamilika mwezi Juni mwaka huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo yaliyobaki katika Mji wa Morogoro yataendelea kupatiwa umeme kupitia bajeti ya TANESCO zinazopangwa mwaka hadi mwaka.