Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 105 2017-02-10

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:-

Katika kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2010 Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga kwa changarawe barabara ya Kibiti – Nyamisati. (a) Je, ni sababu zipi zilizochelewesha kukamilika kwa ahadi hiyo? (b) Je, ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Seif Ungando, Mbunge wa Kibiti, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu za kuchelewa kwa matengenezo ya barabara ya Kibiti – Nyamisati kwa kiwango cha changarawe ni upatikanaji wa fedha. Tathmini iliyofanyika imebainisha kwamba barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 40.8 inahitaji shilingi bilioni 1.2 ili kufanyiwa matengenezo kwa kiwango cha changarawe. Hata hivyo, ili kuifanya barabara hiyo angalau iweze kupitika Serikali katika mwaka wa fedha 2015/2016 iliitengea barabara hiyo shilingi milioni 45.79 kwa ajili ya matengenezo ya kawaida ya kilometa 38.31 na katika mwaka wa fedha 2016/2017 shilingi milioni 24 zilitumika kwa marekebisho ya sehemu korofi yenye urefu wa kilometa mbili na matengenezo ya kawaida ya kilometa 15. (b) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa matengenezo ya barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne, Serikali itajitahidi kutenga fedha za matengenezo kwa awamu ndani ya kipindi hiki cha utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kipande cha kilometa 32.8 kilichobaki baada ya hapo awali kufanyika matengenezo ya kilometa nane kwa kiwango cha changarawe kutoka Kibiti mpaka Ruaruke yaliyofanywa na Wakala wa Barabara Mkoa wa Pwani.