Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 94 2017-02-08

Name

Maida Hamad Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR (K.n.y. MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH) aliuliza:-

Mafuta na gesi ni rasilimali zinazotegemewa kuwa na mchango mkubwa kwa Taifa letu:-
Je, ni aina ngapi za gesi zilizogundulika na faida iliyopatikana tangu ugunduzi huo ulivyotokea?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maida Hamad Abdallah, lililoulizwa na Mheshimiwa Faida Mohammed Bakar, Mbunge wa Chakechake, Pemba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), lilianza utafiti wa masuala ya mafuta na gesi asilia nchini mwaka 1950 ikihusisha utafiti katika maeneo ya baharini ya kina kirefu, maziwa na nchi kavu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, gesi asilia iliyogunduliwa katika maeneo ya bahari ya kina kirefu ni futi za ujazo trilioni 47.08 na katika nchi kavu ni futi za ujazo trilioni 10.17, hivyo kuwa na jumla ya futi za ujazo trilioni 57.25 ya gesi asilia nchini. Gesi asilia iliyogunduliwa ni ya aina moja ya sweet gas, yaani gesi ya kiwango cha juu sana ambayo ina kiwango cha chini sana cha sulfur.
Mheshimiwa Mwenyekiti, faida kubwa iliyopatikana kutokana na ugunduzi wa matumizi ya gesi asilia nchini ni uzalishaji wa umeme wa bei nafuu kwa matumizi ya gesi asilia ikilinganishwa na mafuta. Uzalishaji wa umeme kwa kutumia gesi asilia umeongezeka kutoka unit 2,714.25 kwa mwaka 2014 hadi kufikia unit 4,119 mwaka 2016. Hii ni sawa na asilimia 54.66 ya ongezeko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bei ya umeme imeshuka kutoka wastani wa sh. 188.56 kwa unit mwaka 2014 hadi wastani wa sh. 125.85 kwa unit kwa mwaka 2016, sawa na punguzo la asilimia 33.26. Mbali na punguzo kubwa la umeme, gharama za maombi ya service charge ziliondolewa tangu tarehe mosi Aprili, mwaka 2016, lengo likiwa ni kupunguza gharama za umeme kwa wateja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni ya Helium One imefanya ugunduzi wa gesi ya helium katika maeneo ya Ziwa Rukwa katika bonde la ufa. Kiasi kilichogundulika kinakadiriwa kufikia futi za ujazo bilioni 54. Gesi ya helium hutumika katika matumizi ya mashine za MRI Scanners na vinu vya nuclear katika matumizi ya baluni kwa matumizi ya ndege, hasa kuruka na ndege hewani.