Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 6 | Sitting 4 | Works, Transport and Communication | Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano | 52 | 2017-02-03 |
Name
Joseph Michael Mkundi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Primary Question
MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:-
Ni zaidi ya miaka mitano sasa tangu Meli ya MV Butiama isitishe huduma zake katika Ziwa Victoria kati ya Mwanza na Nansio (Ukerewe) hali inayosababisha shida na usumbufu mkubwa wa usafiri kwa wakazi wa Ukerewe.
(a) Je, ni lini meli hiyo ya MV Butiama itatengenezwa na kuendelea kutoa huduma kati ya Mwanza na Nansio?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta meli mpya hasa ikizingatiwa kuwa meli ya MV Clarius imechakaa sana?
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 3.6 katika bajeti ya mwaka 2016/2017 ili kufanya matengenezo makubwa ya meli ya MV Butiama iliyositisha kutoa huduma zake tangu mwaka 2010 kutokana na hitilafu kubwa ya injini zake. Zabuni kwa ajili ya kupata mkandarasi wa kufanya kazi hiyo zilikwishatangazwa na sasa kazi ya uchambuzi wa kina inaendelea. Matarajio yetu ni mkandarasi kuanza ukarabati huo mwezi Machi, 2017 na kumaliza mwezi Novemba, 2017 (b) Kuhusu mpango wa kujenga meli mpya kwa ajili ya kutoa huduma kati ya Mwanza na Nansio, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuimarisha huduma ya usafiri wa majini katika eneo hilo.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved