Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 39 2017-02-02

Name

Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:-
Jeshi la Zimamoto Mkoani Njombe linakabiliwa na ukosefu wa Ofisi pamoja na vitendea kazi hususan magari jambo linalopelekea Jeshi hilo kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi.
Je, ni lini Serikali italipatia Jeshi hilo ofisi za kudumu pamoja na magari ili liweze kutoa huduma nzuri kwa wananchi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lucia Michael Mlowe, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lina uhaba mkubwa wa ofisi na vitendea kazi katika vituo vyote nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni nia ya Serikali kuongeza bajeti kwa Jeshi la Zimamoto na uokoaji ili liweze kukabiliana na changamoto zilizopo zikiwemo uhaba wa vitendea kazi kama vile magari ya kuzimia moto, magari ya maokozi pamoja na kufanyia ukarabati ofisi zilizopo katika mikoa yote na kuliwezesha Jeshi la Zimamoto kuwa la kisasa ili kutoa huduma nzuri kwa wananchi wote.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo nia hii njema ya Serikali itakuwa ikitekelezwa kwa mujibu wa upatikanaji mapato ya Serikali na bajeti itakayotengwa kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kila mwaka.