Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 2 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 26 2017-02-01

Name

Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING aliuliza:-
Hifadhi ya Kitulo ni muhimu sana kwa Taifa lakini mpaka sasa TANAPA haijaweka miundombinu ya hoteli na barabara ili kuwezesha watalii wanaokwenda Kitulo wawe na mahali pa kukaa:-
(a) Je, ni lini Serikali itawezesha ujenzi wa hoteli ya kitalii katika Tarafa ya Matamba?
(b) Je, ni lini Serikali itawezesha ujenzi wa barabara ya Chimala – Matamba – Kitulo ili kuinua utalii katika Hifadhi ya Kitulo?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Norman Adamson Sigalla, Mbunge wa Makete, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Kitulo inasimamiwa kwa kufuata mpango wa jumla (General Management Plan) wa miaka 10 ulioandaliwa mwaka 2008. Mpango huo umetoa fursa ya kujenga lodge ya vitanda 50 ndani ya hifadhi. Kulingana na taratibu za Hifadhi za Taifa, ujenzi wa huduma za malazi ya aina hiyo hufanywa na sekta binafsi. Serikali itaendelea kuweka kipaumbele katika kutangaza fursa za utalii, hivyo kuvutia uwekezaji katika ujenzi wa miundombinu ya hoteli ili kuboresha shughuli za utalii katika eneo la magharibi na kusini mwa Tanzania ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Kitulo.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Barabara ya Chimala – Matanda – Kitulo ni sehemu ya mipango ya Serikali ya kuendeleza na kusimamia miundombinu inayoelekea kwenye maeneo yenye fursa za kiuchumi. Wizara yangu itaendelea kushirikiana na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ili kuweka kipaumbele katika ujenzi wa barabara zinazoelekea kwenye maeneo yenye vivutio vya utalii zikiwemo za Chimala – Matamba – Kitulo ambayo ni muhimu kwa Hifadhi ya Kitulo, lakini vilevile Iringa – Tungamalenga – Ruaha mahsusi na muhimu kwa Hifadhi ya Ruaha na nyinginezo kwa kiwango cha lami ili kuchochea maendeleo ya utalii.