Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 18 2017-02-01

Name

Hassanali Mohamedali Ibrahim

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Primary Question

MHE. JAKU HASHIM AYOUB (K.n.y. MHE. IBRAHIMU HASSANALI MOHAMMEDALI) aliuliza:-
Wenye maduka waliopewa kibali cha kuegesha magari yao kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi na moja jioni wameonekana wakihodhi nafasi hiyo kwa saa 24:-
(a) Je, ni lini watu wenye tabia hiyo watachukuliwa hatua za kisheria?
(b) Katika Jiji la Dar es Salaam wakati wa usiku inakuwa kama mji huo hauna sheria kwa sababu wenye magari huegesha magari hovyo na kusababisha adha kwa watu wengine. Je, ni lini Serikali itawachukulia hatua watu wa aina hiyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ibrahim Hassanali Mohammedali, Mbunge wa Kiembe Samaki, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria Ndogo ya Maegesho ya Magari GN. Na. 60 ya mwaka 1998 kifungu cha 6(1) kinaipa mamlaka ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Saalam kudhibiti na kusimamia maeneo ya maegesho ya magari yaliyoruhusiwa kwa mujibu wa sheria ili kuondoa kero, usumbufu na msongamano katika mitaa na barabara za umma. Kwa mujibu wa sheria hiyo, maegesho yote ya magari ya kulipia na maegesho yaliyohifadhiwa yanatumika kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni. Baada ya muda huo maeneo hayo huwa huru kwa matumizi ya umma. Pale inapobainika mtu kuhodhi maeneo hayo baada ya saa 12.00 jioni, Halmashauri ya Jiji huchukua hatua kwa mujibu wa sheria.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya ukaguzi na udhibiti wa maeneo ya maegesho imetolewa kwa Mawakala katika Jiji la Dar es Salaam. Napenda kutoa wito kwa wamiliki wote wa magari kuacha kuegesha magari bila utaratibu hasa wakati wa usiku na kusababisha usumbufu kwa watumiaji wengine. Serikali haitasita kuchukua hatua kwa wote watakaobainika kukiuka taratibu za maegesho ya magari katika Jiji la Dar es Salaam kwa sababu kufanya hivyo ni kusababisha msongamano na kero kubwa kwa wengine.