Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Madini 88 2016-11-09

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:-
Serikali ilikuja na mpango mzuri wa umeme Vijijini na kupitia mradi wa REA kukawa na REA I, REA II na sasa REA III na Serikali iliahidi kwamba miradi yote ya REA II ambayo haijakamilika hadi kuanzishwa kwa REA III itatekelezwa sambamba na REA III:-
(a) Je, ni lini Serikali itatekeleza miradi yote ya REA II Jimbo la Chilonwa katika Vijiji vinne vya Kata ya Msamalo(Myunga, Msamelo, Mnase na Mlebe) Vijiji viwili vya Kata ya Zajilwa (Zajilwa na Mayungu) na Kijiji cha Kata ya Manchali?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuviingiza vijiji ambavyo havikuwepo kwenye mpango wa REA II katika mpango wa REA III?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda sasa kujibu swali la Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga, Mbunge wa Chilonwa, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi za kupeleka umeme katika Vijiji vya Kata za Manchali, Msamalo na Zajilwa kupitia mradi wa REA Awamu ya II zitakamilika mwezi Novemba mwaka huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Vijiji vyote vya Jimbo la Chilonwa ambavyo havikupata umeme kupitia REA awamu ya II vitapatiwa sasa umeme kupitia REA Awamu ya III. Kazi ya kupeleka umeme kwenye vijiji hivyo itahusisha ujenzi wa umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 68, ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 301, pia ufungaji wa transformer 45. Mradi huu pia utapeleka umeme kwa wateja wa awali 11,276. Kazi zitaanza mwezi Desemba mwaka huu na kukamilika mwaka wa fedha 2019. Gharama ya mradi huu ni shilingi bilioni 12.09