Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 8 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 92 2016-02-04

Name

Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RIZIKI S. MNGWALI aliuliza:-
Kumekuwa na tatizo sugu nchini kwa baadhi ya vituo vya afya na zahanati kuwa na watumishi wasio na sifa za utabibu:-
Je, Serikali inatumia vigezo gani kuwapeleka watumishi wasio na sifa katika zahanati na vituo vya afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), napenda kujibu swali la Mheshimiwa Riziki Shahari Mngwali, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu ambao unatumika kuajiri watumishi wa kada za afya ni kuwapanga moja kwa moja kwenye vituo vya kazi kadiri wanavyohitimu na ufaulu wa masomo yao. Aidha, ili kuhakikisha watumishi wasio na sifa hawaajiriwi, Serikali imekuwa ikafanya zoezi la uhakiki wa vyeti vyao kabla ya kusaini mikataba ya ajira. Hivyo, endapo Mheshimiwa Mbunge anazo taarifa za kuwepo kwa watumishi wa afya wasio na sifa atusaidie kupata taarifa hizo ili tuweze kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto kubwa ya upungufu wa watumishi wa afya, zipo baadhi ya zahanati na vituo vya afya ambavyo vina watumishi wenye sifa tofauti na muundo. Serikali kupitia Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) inaendelea kushughulikia changamoto hii ambapo tayari mikoa tisa yenye upungufu mkubwa zaidi wa watumishi imetambuliwa na kupatiwa kipaumbele cha kuwaajiri watumishi wa afya. Vilevile Serikali imepanga kuangalia maeneo yenye mlundikano wa watumishi ili kuweka uwiano wa watumishi baina ya zahanati na vituo vya afya vilivyopo mijini na vijijini.