Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Madini 74 2016-11-08

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-
Kwa kuwa Jimbo la Mbogwe limejaaliwa kuwa na madini ya dhahabu na utafiti umekuwa ukiendelea bila uchimbaji kufanyika katika maeneo ya Nyakafuru, Kenegere na kadhalika.
Je, ni lini Wizara ya Nishati na Madini itayaachia maeneo haya na kuyagawa kwa wachimbaji wadogo wadogo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, eneo la Nyakafuru lenye leseni ya ukubwa wa kilometa za Mraba 17.53 linamilikiwa na kampuni ya Mabangu Mining Limited ambayo ni kampuni tanzu ya Resolute Tanzania Limited kupitia leseni PL 5374 ya 2008, leseni hii imeisha muda wake tarehe 23 mwezi wa 10 mwaka huu na kuombewa extension. Hadi sasa mashapo yamefikia tani milioni 3.36 zenye wakia 203,000 za dhahabu yamegunduliwa, na jumla ya dola za Marekani milioni 1.83 zimetumika kufanya utafiti katika eneo la mradi.
Mheshimiwa Spika, eneo la Kenegere lina leseni ya utafiti PL 4582 ya 2007 ambayo imeombewa pia extension kupitia PL 6748 ya 2010. Lakini kuna PL 8329 ya 2012 zinazomilikiwa na kampuni ya Resolute Tanzania Limited ambapo mradi huo kwenye ukubwa wa kilometa za mraba 13.18 upo katika hatua ya upembuzi yakinifu.
Mheshimiwa Spika, kampuni hiyo imetumia zaidi ya dola za Marekani milioni 23 kufanya utafiti na imeainisha mashapu ya dhahabu tani milioni 13 zenye wakia 545,000.
Mheshimiwa Spika, pia eneo la Kanegele lina lesni ya utafiti wa madini PL 10159 ya 2014 yenye ukubwa wa eneo la kilometa za mraba 6.39 pamoja na leseni ya kuhodhi eneo RL 0014 ya 2014 yenye ukubwa wa kilometa za 2.94, kampuni pia inamiliki na leseni ya kampuni ya Resolute Tanzania Limited kupitia kampuni yake tanzu ya Mabangu. Mipango ya uendelezaji wa mgodi katika eneo hilo inaendelea kwa kuzingatia mwenendo wa bei ya dhahabu katika soko la dunia.
Mheshimiwa Spika, ili kutohodhi shughuli za utafutaji zinazoendelea katika eneo hilo Wizara ilishauriana na uongozi wa Wilaya ya Mbogwe tarehe 20 Aprili, 2015 na kuamua kutenga maeneo ya Shenda kwa ajili ya wachimbaji wadogo. Aidha, Kampuni ya Resolute Tanzania Limited imeridhia kutoa leseni ndogo tatu katika eneo la Bukandwa.