Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 5 | Sitting 4 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi | 48 | 2016-11-04 |
Name
Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Busanda
Primary Question
MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:-
Ni Sera ya Taifa kuwa na Chuo cha Ufundi katika kila Wilaya:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha Ufundi katika Wilaya ya Geita?
Name
Eng. Stella Martin Manyanya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Nyasa
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Bukwimba, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza maandalizi ya ujenzi wa Chuo cha Ufundi Standi cha Mkoa wa Geita kitakachohudumia Wilaya zote za Mkoa huo pamoja na maeneo mengine ya nchi. Mnamo tarehe 6 Agosti, 2016 nilifanya ziara katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, moja ya maeneo niliyotembelea ni eneo la Magogo katika Mji wa Geita mahali ambapo chuo hicho kitajengwa. Lengo lilikuwa ni kutoa msukumo wa upatikanaji wa hati miliki ya eneo hilo ili hatua za ujenzi zianze mapema kama ilivyopangwa katika bajeti ya mwaka huu wa 2016/2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo furaha kukuthibitishia kuwa hatimiliki ya kiwanja Namba 177 kitalu E, chenye ukubwa wa hekta 27.27 yaani ekari 68.17 kwa umiliki wa miaka 99 imepatikana. Kazi inayofuata ni kumpata Mshauri Elekezi na Mkandarasi ili ujenzi uweze kuanza mapema iwezekanavyo.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved