Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 9 Good Governance Ofisi ya Rais TAMISEMI. 103 2016-02-05

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:-
Wakati wa Kampeni za Urais mwaka 2015 wananchi wa Momba walipewa ahadi ya kutatuliwa kero ya ushuru wa mazao na mifugo kwenye vizuizi na minada:-
(a) Je, mpaka sasa Serikali imefikia hatua gani katika kushughulikia kero hii?
(b) Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya mwenendo mbovu wa ukusanyaji wa ushuru huo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Ernest Silinde, Mbunge wa Momba lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, ushuru wa mazao hutozwa kwa mujibu wa sheria ya fedha za Serikali za Mitaa Sura Na. 290 kwenye eneo ambalo zao hilo huzalishwa na kuuzwa. Kwa mujibu wa sheria hii ushuru unatozwa kwa mnunuzi wa mazao kutoka kwa mkulima asilimia tatu hadi asilimia tano ya bei ya gharama (farm gate price). Aidha, kwa upande wa ushuru wa Mifugo, ushuru huu hutozwa mnadani au sokoni baada ya mifugo kununuliwa.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inasisitiza na kuwataka Wakurugenzi wote wa Halmashauri kuhakikisha kuwa wanazingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia utaratibu wa utozaji na ulipaji wa kodi katika ushuru husikia.