Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 4 Finance and Planning Ofisi ya Rais TAMISEMI. 43 2016-11-04

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatambua mchango mzuri wa wasimamizi wa Rasilimali Fedha, Wahasibu Viongozi (Chief Accountants) walioko kwenye Wizara na Idara za Serikali kwa kuwapandisha kwenye ngazi ya Ukurungenzi ili waweze kuleta tija zaidi kwa ushirika wao katika maamuzi ya Menejimenti ya Wizara/Idara zao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Elias John Kwandikwa, Mbunge wa Jimbo la Ushetu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, cheo cha Mhasibu Mkuu au Chief Accountant ni cheo cha madaraka/uongozi na kwa mtumishi anayeteuliwa kushika wadhifa huu anakuwa na hadhi sawa na Mkuu wa Idara au Mkurugenzi katika Wizara au Idara ya Serikali inayojitegemea au wakala na Wahasibu Wakuu ni sehemu ya Menejimenti ya Wizara, Wakala, Idara za Serikali zinazojitegemea na wamekuwa wakishiriki kikamilifu katika maamuzi ya Wizara na Idara zao kama ambavyo wako Wakuu wengine wa Idara au Wakurugenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuwapatia mafunzo ya awali watumishi na viongozi wa umma kabla ya uteuzi wa madaraka yoyote katika utumishi wa umma ili waweze kuuelewa utumishi wa umma na kufahamu misingi, sheria, kanuni na taratibu za utendaji kazi katika utumishi wa umma. Mafunzo ya aina hii yamekuwa yakitolewa na Taasisi ya Uongozi, Chuo cha Utumishi wa Umma pamoja na wakala wa mafunzo kwa njia ya mtandao au (TAGLA).