Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 4 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 41 2016-11-04

Name

Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA aliuliza:-
Hospitali ya Wilaya ya Mbinga inatoa huduma kwa Halmashauri Nne yaani Mbinga Mjini, Mbinga Vijijini, Nyasa na baadhi ya Kata za Songea Vijijini, hali inayopelekea Hospitali hiyo kuwa na upungufu wa vitendeakazi, wodi na vyumba vya kulaza wagonjwa pamoja na ukosefu wa Madaktari Bingwa:-
Je, ni lini Serikali itaboresha Hospitali hiyo ili iweze kutoa huduma inayotarajiwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sixtus Raphael Mapunda, Mbunge wa Mbinga Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kutatua tatizo la vitendea kazi, Serikali inashirikiana na wadau mbalimbali ili kuboresha huduma za afya. Serikali kupitia wadau ambao ni wattereed imefanikisha upatikanaji wa gari la wagonjwa lenye namba DFP 5795 ambalo linatumika kuhudumia wagonjwa wanaohitaji rufaa. Wadau hao pia wamesaidia upatikanaji wa mashine muhimu za kupima CD4 na maradhi ya kifua kikuu pamoja na kuwezesha ukarabati wa jengo la maabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali hiyo inakabiliwa na upungufu wa wodi ya watoto na ufinyu wa wodi ya wazazi. Aidha, majengo ya wodi ya upasuaji, wodi ya wanaume, wodi ya daraja la kwanza na kliniki ya meno ni chakavu. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali imetenga shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya watoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mahitaji ya Madaktari (Medical doctors) katika hospitali ni nane, waliopo ni wawili na upungufu ni madaktari sita. Aidha, Madaktari wasaidizi wanaohitajika ni 16, waliopo ni sita na upungufu ni Madaktari 10. Halmashauri imepata kibali cha kuajiri Madaktari wanne katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016. Madaktari watatu waliokuwa masomoni wanatarajiwa kuripoti kazini mwaka huu 2016.