Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 2 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 24 2016-11-02

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA aliuliza:-
Katika Kijiji cha Isenzanya Wilayani Mbozi, shamba lenye ukubwa wa hekari 1,000 linalohodhiwa na Mzungu aitwaye Joseph Meya halijaendelezwa kwa miaka mingi sasa huku wananchi wa kijiji hicho wakiwa hawana maeneo ya kilimo:-
Je, Serikali haioni ni wakati muafaka wa kulirejesha shamba hilo kwa wananchi?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA (K.n.y. WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Pascal Yohana Haonga, Mbunge wa Jimbo la Mbozi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bwana Joseph Meier na Bi. Enala Mgala kwa pamoja wanamiliki shamba lenye ukubwa wa hekta 330.16 ambayo ni sawa na ekari 825.4 kwa Hati Na. 257 MBY LR lililopo katika Kijiji cha Isenzanya, Wilaya ya Mbozi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba wamiliki hawa wameendeleza kipande kidogo cha shamba hili kwa kupanda kahawa na mazao ya msimu kama mahindi na maharage. Hata hivyo, kutokana na mahitaji ya ardhi kuongezeka, wananchi wa Kijiji cha Isenzanya kwa nyakati tofauti kupitia kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi wamekuwa wakiiomba Serikali kuwapatia ardhi hiyo ili waitumie kwa kilimo. Katika kutekeleza azma hiyo, November 2015 Mkurugenzi wa Halmashauri alifanya mkutano uliojumuisha wamiliki na wanakijiji wa Kijiji cha Isenzanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mkutano ukaguzi wa shamba kufanyika mpaka sasa mazungumzo na wamiliki wa shamba yanaendelea. Aidha, Sheria ya Ardhi, Namba 4 ya Mwaka 1999 imeeleza wazi namna ya utoaji wa maeneo pale ambapo mmiliki anakiuka masharti yake. Halmashauri kupitia Afisa Ardhi Mteule inayo mamlaka ya kusimamia utekelezaji wa sheria husika. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge awe na subira wakati Serikali ikiendelea na utaratibu wake.