Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Madini 14 2016-11-01

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:-
Serikali imekuwa na ahadi nyingi, nzuri za kutekeleza katika kusambaza umeme kwenye maeneo mengi ya nchi yetu.
(a) Katika Wilaya ya Nyang‟hwale ni vijiji vitatu tu vya Nyang‟hwale, Nyarubele, Busegwa na Makao Makuu ya Wilaya ambavyo vina umeme; je, katika bajeti ijayo ni vijiji vingapi vya Jimbo la Nyang‟hwale vitapatiwa umeme?
(b) Je, kwa nini nguzo haziletwi Kharumwa wakati wateja wengi tayari wamefanya wiring kwenye nyumba zao?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Nyang‟hwale lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya vijiji 61 katika jimbo la Nyang‟hwale vitapatiwa umeme katika utakekezaji wa mradi kabambe wa REA Awamu ya Tatu. Kazi ya kupeleka umeme kwenye vijiji hivyo itajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovolt 33 yenye urefu wa kilometa 50, ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovolt 0.4 yenye urefu wa kilometa 372 na ufungaji wa transformer 24 pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 3,578. Kazi hizi zitaanza mwezi Disemba mwaka huu na kukamilika mwaka wa fedha 2019/2020. Gharama ya mradi huu ni shilingi bilioni 6.23.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji cha Kharumwa ambacho ni makao makuu ya Wilaya ya Nyang‟hwale tayari kimepatiwa umeme na kazi ya kupeleka nguzo inaendelea. Hata hivyo TANESCO inakamilisha kazi za kuunganishia umeme wateja wapya wa Kharumwa kadri maombi yatavyofikiwa. Mpaka mwisho wa mwezi wa Disemba mwaka huu vijiji vya Kharumwa vitakuwa vimepata umeme.