Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 1 Water and Irrigation Ofisi ya Rais TAMISEMI. 07 2016-11-01

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kusambaza maji katika Kata za Kasamwa, Shiloleli, Bulela, Nyarugusu, Bukeli na maeneo mengine ya Wilaya ya Geita na Mkoa wa Geita kwa ujumla?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Upendo Furaha Peneza, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Geita kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 imepanga kutumia shilingi milioni 593.14 kwa ajili ya kuboresha huduma za maji katika Kata za Kasamwa, Shiloleli, Bulela, Nyarugusu na Bukolina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi zitakazofanyika ni ujenzi wa miundombinu ya maji kwa kutumia chemchemi ya Mawemeru katika Kata ya Nyarugusu; uchimbaji wa visima virefu katika Kata ya Bulela na Shiloleli na kuboresha miundombinu ya maji iliyopo katika kata ya Kasamwa na Kanyara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wa mzima wa Geita Serikali imepanga kutumia shilingi bilioni 8.9 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji ambazo zimetengwa katika bajeti ya mwaka 2016/2017. Fedha hizo zitatumika kujenga miradi ya maji 22 ili kuboresha huduma ya maji kwa wananchi.