Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 4 | Sitting 8 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii | 110 | 2016-09-16 |
Name
Hawa Abdulrahiman Ghasia
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Mtwara Vijijini
Primary Question
MHE. HAWA A. GHASIA aliuliza:-
Je, Serikali imeweka mikakati gani ili kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Kanda ya Kusini inayojengwa Mikindani Mtwara?
Name
Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nzega Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Abdulrahman Ghasia, Mbunge wa Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Kanda ya Kusini, Wizara inaendelea kushirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo katika sekta ya afya ili waweze kuchangia gharama za kukamilisha mradi huu. Vilevile Wizara inaendelea kufanya majadiliano na taasisi mbalimbali za Serikali ambazo zinaweza kutoa mkopo wenye masharti nafuu kwa ajili ya ukamilishaji wa mradi huu.
Hata hivyo, katika Bajeti ya mwaka 2016/2017, Wizara imetenga jumla ya shilingi bilioni mbili kwa ajili ya kuanza kwa awamu nyingine ya ujenzi wa majengo mengine ya kutolea huduma baada ya kukamilika kwa jengo la matibabu ya magonjwa ya nje (Out Patient Department) na mapokezi.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved