Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 4 | Sitting 8 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi | 107 | 2016-09-16 |
Name
Rwegasira Mukasa Oscar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Biharamulo Magharibi
Primary Question
MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:-
Biharamulo ni moja ya Wilaya za Mkoa wa Kagera zilizoathirika sana na ugonjwa wa mnyauko wa migomba na hivyo ustawi wa zao hilo kuu la chakula upo mashakani.
Je, Serikali inatoa kauli gani isiyo nyepesi na inayolingana na uzito wa suala hili?
Name
William Tate Olenasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ugonjwa wa unyanjano unasababishwa na bakteria aitwaye Bacterium Xanthomonas Campetris pv. Musacearum. Serikali inaendelea kufanya juhudi za kuudhibiti na kuzuia ugonjwa huu nchini kwa kutoa elimu sahihi juu ya unyanjano kwa wadau wote, madhara, ueneaji na udhibiti wa ugnjwa huu. Maeneo ambayo yamezingatia maelekezo ya udhibiti yamefanikiwa kupunguza kasi ya kusambaa kwa ugonjwa huu. Hata hivyo katika kipindi cha ukame ugonjwa wa black sigatoka umejitokeza Wilayani Biharamulo na kuleta athari kubwa katika zao la migomba. Ugonjwa huu unasababishwa na Fungi. Ugonjwa huu umejitokeza kuanzia mwezi wa Juni mwaka 2016 baada ya kuanza kipindi cha jua. Maeneo yaliyoathirika ni Nyamahanga vijiji vinne, Bisibo vijiji vinne, Ruziba vijiji vinne, Rusahunga vijiji vinne na Biharamulo vijiji vinne.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara kupitia kituo chake cha utafiti kimeelekeza wataalam wa kilimo Wilayani Chato kuwashauri wakulima, kuondoa migomba yenye dalili kali za ugonjwa huo na kupanda mbegu aina ya FHIA zinazovumilia ugonjwa huu ambazo kwa sasa mbegu hizi zinapatikana kwa wingi Wilayani humo. Wakulima wakizingatia ushauri huo utasaidia kupunguza usambaaji wa ugonjwa huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, magonjwa ya unyanjano na black sigatoka yanaweza kutokomea iwapo wakulima watafuata kanuni bora za kilimo. Aidha, watafiti wetu na wa nchi za Kanda za Afrika Mashariki wanaendelea kutafiti aina ya migomba yenye ukinzani dhidi ya ugonjwa huu.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved