Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 4 | Sitting 8 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa | 96 | 2016-09-16 |
Name
Selemani Jumanne Zedi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukene
Primary Question
MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:-
Ukosefu wa nyumba za walimu katika maeneo ya vijijini unasababisha Walimu kuhama maeneo hayo na hivyo kusababisha upungufu mkubwa wa Walimu, pia Halmashauri nyingi hazina uwezo wa kujenga nyumba za Walimu za kutosha kwa kutumia fedha zao za ndani.
Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga nyumba za Walimu wa shule za msingi vijijini hasa ikizingatia kuwa vijijini hakuna nyumba ambazo Walimu wanaweza kupanga?
Name
Selemani Said Jafo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisarawe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi Mbunge wa Jimbo la Bukene kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa nyumba za Walimu kupitia bajeti zilizotengwa katika kila mwaka. Katika mwaka wa fedha 2016/2017, Serikali imetenga shilingi bilioni 13.9 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 1,157 kwa shule za msingi na shilingi bilioni 11.1 zimetengwa kujenga nyumba 661 kwa shule za sekondari nchini. Aidha, kupitia mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES II), Serikali imepanga kujenga nyumba za Walimu 183 katika shule za sekondari kwenye Halmashauri mbalimbali zenye uwezo wa kuchukua familia sita kwa kila nyumba.
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Nzega katika mwaka wa fedha 2016/2017 imetengewa shilingi milioni 486.3 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Walimu kwa shule za msingi na sekondari.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved