Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 5 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 68 2016-09-13

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:-
Baada ya ukarabati wa Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi vya FDC – Njombe na kile cha Ulebwe kilichopo Wanging‟ombe.
(a) Je, ni fani zipi zitaanza kutolewa katika vyuo hivyo?
(b) Je, ni wananchi wangapi wanatarajia kufaidika na vyuo hivyo?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edward Franz Mwalongo, Mbunge wa Njombe Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya ukarabati wa Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (FDC) Njombe na kile cha Ulebwe kilichopo Wanging‟ombe, Serikali itaendelea kuimarisha na kutoa mafunzo yale yale yaliyokuwa yanatolewa hapo awali, yaani mafunzo ya ufundi stadi katika fani za ufundi magari, ufundi chuma, useremala, uashi, umeme wa majumbani, ushonaji, kilimo na mifugo katika Chuo cha Njombe na fani za useremala, ushonaji, uashi, umeme wa majumbani, kilimo na mifugo katika Chuo cha Ulebwe.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kulingana na uwezo na vyuo hivyo, Chuo cha Mendeleo ya Wananchi Njombe kina uwezo wa kunufaisha wananchi 180 wa kukaa bweni na wananchi 70 wa kutwa, wakati Chuo cha Wananchi Ulebwe kina uwezo wa kunufaisha wananchi 80 wa kukaa bweni na 40 wa kutwa na hivyo kufanya jumla ya wananchi wanufaika 370 kwa mwaka.