Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 77 2016-09-14

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Primary Question

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL aliuliza:-
Mafunzo na mazoezi ya kijeshi yanayofanywa na Chuo cha Polisi (CCP) katika eneo la Kata ya Donyomorwa katika Wilaya ya Siha yamesababisha maafa makubwa kwa wananchi ikiwa ni pamoja na wananchi kuuawa kwa risasi na mabomu yanayotumika katika mazoezi hayo.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhamisha mafunzo hayo kutoka kwenye maeneo ya makazi ili kuepusha maafa yanayowapata wananchi wa maeneo hayo?

Name

Charles Muhangwa Kitwanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Godwin Oloyce Mollel, Mbunge wa Siha, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haina mpango wa kuhamisha mafunzo ya kijeshi katika eneo la Donyomorwa. Awali mafunzo hayo yalikuwa yakifanyika katika eneo la Kilelepori ambalo lilivamiwa na wananchi kwa kujenga nyumba na kufanya shughuli za kilimo ambapo Serikali iliamua kuhamisha mafunzo ya kijeshi katika eneo hili nililolitaja sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuepusha madhara yanayoweza kuwapata wananchi, Serikali itaendelea kutoa elimu kwa jamii ya Kimasai kuacha kuchunga mifugo katika eneo hilo, kukata kuni na kuokota kitu chochote wasichokijua katika eneo hilo. Aidha, kabla ya Polisi kuanza mazoezi ya kijeshi huchukua tahadhari kama kutoa taarifa kwa Vijiji, Wilaya na Mkoa ikiwa ni pamoja na kuweka alama za tahadhari kuzunguka eneo lote kwa kuweka bendera nyekundu na kuwaweka askari katika vipenyo vya kuingia katika eneo hilo.