Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Madini 79 2016-09-14

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Primary Question

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA aliuliza:-
Mradi wa REA umekuwa ukisuasua katika maeneo ya vijiji vya Rufiji hususan Tarafa ya Mkongo, Kata za Mkongo, Ngorongo, Kipungila na Kata ya Mwaseni na Ngarambe.
Je, ni lini mradi huo utakamilika katika hatua inayofuata?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa, Mbunge wa Rufiji, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa REA Awamu ya III ambao utafuata sasa na ambao unatekelezwa baada ya Mradi wa REA Awamu ya II katika Wilaya ya Rufiji unatekelezwa na Mkandarasi MBH Power Ltd. Wigo wa kazi katika Wilaya hii unahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 217.34; ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 04 yenye urefu wa kilometa 64.18; ufungaji wa transfoma 40 na kuwaunganishia umeme wateja wapatao 2,059.
Mradi umekamilika kwa asilimia 76 zikijumuisha ujenzi wa kilometa 201 za msongo wa kilovoti 33; ujenzi wa kilometa 23 za msongo wa kilovoti 0.4; kufunga transfoma 17 pamoja na kuwaunganishia umeme wateja 256. Mradi huu hadi kukamilika utagharimu shilingi bilioni 7.74.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata za Mkongo, Ngorongo, Kipungila, Mwaseni na Ngarambe ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 94 kutoka Ikwiriri hadi Mloka umekamilika kwa asilimia 90. Ujenzi wa njia ya usambazaji umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu kilomita 24.64 imekamilika kwa asilimia 45 na ufungaji wa transfoma 14 unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Septemba 2016. Kazi hizi zinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Oktoba, 2016. Kazi hii hadi kukamilika itagharimu shilingi bilioni 3.15.