Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 36 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 301 2016-06-03

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE.ALLY K. MOHAMED aliuliza:-
Vituo vya Polisi vya Kabwe na Kirando vimechakaa sana na hata polisi hawana nyumba za kuishi:-
Je, ni lini Serikali itajenga au kukarabati vituo hivyo na kuwajengea polisi nyumba za kuishi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Keissy, Mbunge wa Nkasi Kaskazini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango wa kukarabati, kujenga makazi na vituo vya Polisi nchi nzima ikiwemo Kabwe na Kirando kwa awamu. Kwa upande wa makazi ya Askari Polisi awamu ya kwanza ya ujenzi itajumuisa nyumba 4,136. Kwa vituo ambavyo ni chakavu Serikali itaendelea kuvifanyia ukarabati kulingana na uwezo wa fedha kadri utakavyoruhusu.