Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 67 2016-02-02

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. RICHARD M. NDASSA aliuliza:-
Miradi ya umeme ya REA Awamu ya Kwanza na ya Pili inaendelea vizuri.
Je, ni lini miradi ambayo haijakamilika itakamilika hasa ikizingatiwa kuwa Serikali iliahidi kukamilika kwa miradi hiyo kabla ya tarehe 30 Juni, 2015?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Richard Mganga Ndassa, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilifadhili utekelezaji wa mradi kabambe wa kusambaza umeme vijijini, Awamu ya Kwanza na ya Pili kupitia Mfuko wa Nishati Vijijini (REA). Miradi ya awamu ya kwanza imeshakamilika kwa asilimia mia moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, jumla ya fedha iliyotengwa kutekeleza miradi ya REA Awamu ya Pili ni shilingi bilioni 877.3 na hadi sasa Serikali imeishalipa asilimia 75 na inaendelea kutoa fedha ili miradi ikamilike kabla ya mwezi Juni, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Awamu ya Pili, katika Mkoa wa Mwanza ikiwemo Jimbo la Sumve Wilaya ya Kwimba unatekelezwa na Mkandarasi Chico-CCC (BV) JV. Wigo wa kazi wa Mkoa wote kwa Mwanza ni ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 wenye urefu wa kilomita 463. Kadhalika ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 365 na kuunganisha umeme wateja wa awali wapatao 8,990. Utekelezaji wa kazi wa Mkoa wa Mwanza umefikia asilimia 78. Gharama ya Mradi wote wa REA Phase II ni shilingi bilioni 25.36. Mradi unatalajiwa kukamilika kabla ya mwezi Juni mwaka huu.