Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 38 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 320 2016-06-07

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA (K.n.y. MHE. RHODA E. KUNCHELA) aliuliza:-
Kumekuwa na sintofahamu katika eneo la Kata ya Misunkumilo, Wilaya ya Mpanda Mjini, Wanajeshi wanadai eneo hilo ni la Jeshi, lakini makazi ya wananchi yalitangulia na wana hati ya maeneo yao:-
Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutatua jambo hili ikiwa Jeshi limewakuta wananchi katika eneo hili?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rhoda Edward Kunchela, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na sababu za kistratejia, JWTZ lilipewa eneo la Misunkumilo lililopo Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mwaka 1985 lenye ukubwa wa hekta 3195. Serikali ililipa fidia kwa wananchi waliokuwepo katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 1992 Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania lilihamisha kombania yake kutoka katika eneo hilo ila eneo alikabidhiwa Mkuu wa Wilaya kwa uangalizi. Kutokana na sababu za kiusalama hasa ukanda wa Ziwa Tanganyika, imebidi Jeshi lirejee kwenye sehemu hiyo tena. Hata hivyo, sehemu ya eneo hili sasa limevamiwa na kupangiwa matumizi mengine na uongozi wa Manispaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 16 Novemba, 2015 kilifanyika kikao cha pamoja kati ya JWTZ na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Katavi. Maamuzi yaliyofikiwa katika kikao hicho ni kulipima upya eneo hilo kwa kuzingatia maendeleo yaliyopo, lakini vile vile na mahitaji ya JWTZ.
Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi eneo hili litapungua kutoka ekari 3,195 za awali hadi 2,235. Zoezi la kupima upya litakuwa shirikishi na litatekelezwa mara fedha zitakapopatikana katika mwaka wa fedha wa 2016/2017.