Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 48 2016-09-09

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:-
Serikali ya Awamu ya Tano inakusudia kuifanya Tanzania kuwa ni nchi yenye uchumi wa viwanda, hivyo inahitaji kuwa na uzalishaji wa umeme wa uhakika. Hata hivyo, umeme unaozalishwa kwa kutumia gesi asilia pale Somanga Fungu unakatika mara kwa mara na kusababisha adha kubwa kwa watumiaji:-
Je, Serikali inaweza kutuambia wananchi kiini hasa cha ukatikaji huo wa kila siku wa umeme unaozalishwa kutokana na gesi ya Songosongo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vedasto Edgar Ngombale, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Somanga Fungu kilianza kuzalisha umeme mwaka 2010. Kituo hicho kina jumla ya mitambo mitatu ya kuzalisha umeme kiasi cha Megawati 7.5 kwa kutumia gesi asilia. Umeme unaofuliwa kutoka Somanga Fungu unatumika katika Wilaya za Kibiti, Kilwa pamoja na Rufiji. Kwa sasa mtambo mmoja wenye uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 2.5 pia haufanyi kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kukatika kwa umeme ni kweli kabisa kumekuwa na kukatika kwa umeme katika Wilaya za Kilwa, Kibiti pamoja na Rufiji kunakosababishwa na hitilafu katika mitambo ya kuzalisha umeme pamoja na miundombinu ya kusambaza umeme. Ili kukabiliana na changamoto hiyo tunaimarisha upatikanaji wa umeme katika wilaya hizo na Serikali kupitia TANESCO imeanza ukarabati sasa, ambao ni overhaul kabisa wa mitambo miwili ya uwezo wa kuzalisha umeme wa jumla ya megawati tano.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia tunafanya ukarabati na kufunga mtambo mwingine kwenye mtambo unaozalisha megawati mbili na kufanya sasa jumla ya gharama za marekebisho pamoja na kufunga mtambo kufikia bilioni tano. TANESCO inaendelea na ukaguzi, inafanya usafishaji na ukarabati wa mitambo hiyo ili kuwahakikisha wananchi wa maeneo hayo wanapata umeme wa uhakika.