Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 42 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 358 2016-06-14

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-
Sekta ya utalii ina mchango mkubwa katika kuliingizia Taifa fedha za kigeni:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya barabara, hoteli na airstrips katika Pori la Akiba la Kigosi ili kuweza kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea vivutio vilivyopo katika Pori hili zuri la Kigosi na Muyowosi?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mchango wa sekta ndogo ya utalii katika uchumi wa Taifa na maendeleo ya jamii ni mkubwa sana hususan kwa kuongoza katika kuipatia Serikali fedha nyingi za kigeni na pia kuchangia Pato la Taifa kwa ujumla kwa kiwango cha asilimia 17. Aidha, Wizara yangu inaamini kwamba kwa kuboresha miundombinu, vivutio na utoaji huduma, sekta hii inaweza kuchangia zaidi katika Pato la Taifa na upatikanaji wa fedha za kigeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mapori ya Akiba ya Moyowosi na Kigosi yenye jumla ya kilometa za mraba 21,060 yanapakana na Mikoa ya Kigoma, Shinyanga na Geita. Eneo kubwa la mapori hayo ni ardhi oevu ambayo inawezesha upatikanaji wa maji kwa kipindi chote cha mwaka kwa ajili ya ustawi wa wanyamapori. Mapori haya ni moja kati ya maeneo ya mkakati ya Wizara katika kuinua utalii wa Kanda ya Magharibi na Kanda ya Ziwa Magharibi ambapo kwa sasa yanatumika kwa shughuli za utalii wa uwindaji. Aidha, baadhi ya maeneo ndani ya mapori haya yana rasilimali za wanyamapori na uoto wa asili mzuri unaofaa kwa shughuli za utalii wa picha na hivyo kuhitaji uboreshaji wa miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya 3(c) ya Ilani ya CCM 2015 – 2020 inasisitiza juu ya umuhimu wa suala hili na inaelekeza Serikali kuboresha miundombinu ndani ya mapori ya akiba ikiwa ni mojawapo ya mikakati ya kuhakikisha kwamba mazao yatokanayo na maliasili yanaendelea kuchangia katika ukuaji wa uchumi na fursa za ajira katika kuwaongezea wananchi kipato.