Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 23 Industries and Trade Maswali kwa Waziri Mkuu 4 2016-05-19

Name

Lucy Simon Magereli

Gender

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY S. MAGERELI:
Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la moja kwa moja kwa Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Waziri Mkuu , Mpango wa Serikali wa Miaka Mitano ni kuipeleka Tanzania kuwa Tanzania ya viwanda na ziko changamoto zinazokabli mpango huo na moja ni namna ya kuwawezesha wazalishaji na wafungashaji wadogo katika level za Halmashauri kufanya kazi hiyo kwa ufanisi mkubwa.
Tunafahamu uwepo wa GS1 ambayo inalengo la kuwasaidia wazalishaji na wafungashaji hao kupata barcodes ili waweze kuuza bidhaa zao. Mwaka jana Waziri Mheshimiwa Mizengo Pinda alitoa maelekezo ya maandishi akielekeza TAMISEMI iagize halmashauri zote zitoe
ushirikiano kwa GS1 ili waweze kuwasaidia hao wazalishaji na wafungashaji wadogo kupata barcodes kitu ambacho kinge-stimulate uanzishwaji wa viwanda vidogo vidogo...
SPIKA:
Mheshimiwa Lucy sasa swali.
MHE. LUCY S. MAGERELI:
Mheshimiwa Spika ahsante, ningetemani nimalizie, anyway.
Nini sasa Kauli ya Serikali hasa kwa Ofisi ya Waziri Mkuu katika kusimamia na kutekeleza maelekezo haya ambayo tayari yalishatolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu aliyepita ili kuwasaidia wazalishaji na wafungashaji wadogo hawa?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Ni kweli kwamba Serikali inayo mkakati, tunaendelea kuhamasisha wajasiriamali wadogo kujiendeleza kupitia viwanda vidogo vidogo na msisitizo huu wa Serikali wa viwanda unajumuisha viwanda vikubwa, vya kati na vidogo kwa lengo lile lile la kumtaka Mtanzania aweze kunufaika na hasa katika kuongeza thamani ya mazao ambayo tunayazalisha nchini.
Tumeendelea kuwa na mipango mbalimbali ambayo Serikali inaunga mkono jitihada za wazalishaji wadogo ikiwemo na uwekaji wa barcodes ambayo pia inamsaidia kupata bei na thamani nzuri ya mazao ambayo mjasiriamali anajihusisha katika kuchakata kwenye michakato ya awali kwa maana processing hii ya awali.
Mheshimiwa Spika, mkakati huu bado unaendelea na tumeagiza utaratibu huu wa
barcodes uendelee lakini pia tumehusisha TBS, TFDA kuhakikisha kwamba chakula tunachokizalisha kinakuwa na ubora ili tukikipa barcode, Taifa liweze kuuza bidhaa hiyo nje ya nchi na ndani ya nchi ambako tunaweza kupata fedha nyingi na wajasiriamali waweze kunufaika zaidi.
Kwa hiyo, nataka nikuhakikishie tu kwamba utaratibu huo bado unaendelea ili kuweza kuipa thamani mazo yetu lakini kuwapa uwezo mkubwa wa kusafirisha bidhaa zao nje na kuzipa soko ili ziweze kuwaletea tija Watanzania na tutaendelea pia kusimamia jambo hilo kuwa linaendelea kukamilika. Ahsante sana.

Additional Question(s) to Prime Minister

Name

Lucy Simon Magereli

Gender

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Question 1

MHE. LUCY S. MAGERELI:
Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, nilichotamani kusikia kutoka kwako ni tamko lako kama Serikali kuziagiza Halmashauri kutoa ushirikiano kwa
GS1 lakini TFDA, TBS na washirika wengine ikiwemo Wasajili wa Viwanda wa Makampuni kwa sababu hiyo ni timu inayofanya kazi pamoja. Changamoto hiyo imekuwa kubwa kwa sababu ya kupata
resistance kutoka kwa Halmashauri, lengo mlilolianzisha lilikuwa jema lakini Halmashauri hazitoi ushirikiano na kutotoa ushirikiano zinawanyima fursa wazalishaji na wafungashaji wadogo kupata fursa hiyo.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nimekusikia kwa namna ambavyo ume-experience
huko ambako umeona kwamba Halmashauri zetu hazitekelezi maagizo yetu ambayo tunayatoa na inawezekana siyo Halmashauri tu ziko pia nyingine ambazo pia zinafanya jambo hilo hilo. Kwa hiyo, nilichukue jambo lako baada ya kikao hiki nitawasiliana na Waziri wa TAMISEMI kuhakikisha kwamba maagizo yetu ya Serikali yanatekelezwa na wazalishaji wetu wadogo wanapata nafasi.
Lakini pia Wizara ya Kilimo nayo pia ilichukue hili kwa sababu tunayo
Maonesho ya Kilimo ambayo sasa tumeyaanzisha katika kanda mbalimbali, hawa wajasiriamali wadogo wapate nafasi za kwenda kuonyesha bidhaa zao kwenye maonyesho yale ili pia waweze kutangaza soko lao, waonyeshe ubora wao na sasa Halmashauri zisimamie wajasiriamali wadogo hao kwenda kwenye maonyesho hayo ili uonyesha kazi zao ziweze kuleta tija zaidi huo ndiyo msisitizo wa Serikali.
(Makofi)