Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 21 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 1 2022-05-12

Name

Iddi Kassim Iddi

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mheshimiwa Waziri Mkuu kumekuwepo na ongezeko la mizani za kupimia mizigo ya magari nchini kote na hivyo kuongeza idadi kubwa ya watumishi katika mizani hizo, ambao kimsingi hawa mikataba ya kudumu. Sasa ukosekanaji wa mikataba ya kudumu inasababisha kukosekana kwa haki yao msingi kukopa. Nini kauli ya Serikali na hasa ukizingatia ajira hizi mpya watumishi kupata ajira za kuduma?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Msalala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali imeongeza huduma za upimaji wa uzito wa magari nchini ambako tunavyo vituo maalum vilivyojengwa, lakini pia tunazo mizani zinazotembea kwa lengo la kuhakiki uzito wa magari ili yanapopita kwenye barabara zetu tusipate uharibifu mkubwa, kwa kuongeza mizani pia tumeongeza watumishi waliopo chini ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, sasa watumishi hawa ni sehemu ya watumishi wote ambao wanapata mikataba yao.

Mheshimiwa Spika, iko mikataba ya muda mfupi, iko mikataba ya kudumu na tunafanya hilo ili kuwezesha pia watumishi hao kuwa na stahiki zao za kimsingi. Sasa ni lini tutaweza kuimarisha mikataba hiyo ili wapate haki zao za kudumu pamoja na stahiki zingine ikiwemo mikopo na haki nyingine, hili linategemea pia na nafasi za ajira Serikali na nafasi ambazo zinapewa sekta ya ujenzi kwenye mizani ili kuweza kuwaajiri moja kwa moja watumishi hawa.

Mheshimiwa Spika, ninalichukua hilo na Waziri wa Uchukuzi yuko hapa anasikia, kwa hiyo, ni jukumu sasa la kuratibu vizuri watumishi wote wanaofanya kazi kwenye mizani wenye mikataba ya muda mfupi kuona kama wanazo sifa za kupata ajira za kudumu ili wapate mikata ya kudumu na hatimaye haki zao ziweze kusaidiwa. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister