Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 8 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2023-02-09

Name

Zaytun Seif Swai

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, nyakati mbalimbali tumeona Serikali yetu ikitoa misamaha ya kodi kwenye bidhaa zile muhimu ili basi kupunguza gharama kwa wananchi wetu. Mwaka 2019 tuliona msamaha wa kodi kwenye taulo la kike, lakini bei ya soko haikupungua na mwaka 2021 tuliona msamaha wa kodi kwenye simu janja, lakini bei ya soko haikuweza kupungua.

Je, ni ipi mikakati ya Serikali kwenye kudhibiti bei ya soko, pale ambapo misamaha hii ya kodi inapotolewa? Ahsante.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika naomba kujibu swali la Mheshimiwa Swai, Mbunge wa Arusha kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, upo ukweli kwamba Serikali inao mfumo wa kutoa misamaha ya kodi pale ambako inajiridhisha kwamba eneo hilo linaloombewa msamaha linaweza pia kupewa msamaha huo na hiyo inatakana pia na mtizamo wetu ndani ya Serikali kwamba kunaweza kuwa kuna maslahi, maslahi hiyo inaweza kuwa ni pamoja na ambalo Mheshimiwa Mbunge amelisema la kupunguiza gharama ya bidhaa hiyo au ya huduma hiyo.

Mheshimiwa Spika, mfano hivi karibuni tumeona kupanda kwa bei ya mbolea nchini na Serikali ilipogundua kwamba gharama ya kununua mbolea ya shilingi 110,000 au zaidi ni kubwa na kwamba Watanzania hawawezi kumudu kununua na kwamba ili kuleta maslahi kwa Watanzania, Serikali ilitoa msamaha wa kodi, wakati mwingine pia na kutoa ruzuku na kuwezesha kupunguza gharama ya upatikanaji wa bidhaa hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Serikali inaendelea na utaratibu huu pale ambako inaona kuna bidhaa au huduma yenye maslahi na tunaweza tukaamua au mtu anayetoa huduma hiyo akaomba msamaha wa kodi na msamaha ukitolewa matarajio yetu ni kuona kuwa gharama hiyo inapungua.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Serikali itaendelea kuhakikisha kwamba maeneo yote haya ambayo yanapata ruzuku, yanapewa msamaha wa kodi, tunayasimamia kuwa na maslahi kwa watumiaji, kwa Watanzania kwa sababu unaposema unatoa msamaha wa kodi lile pengo la fedha lililokuwa linatakiwa kuuzwa awali na hii ya sasa baada ya msamaha linalipiwa pia na Serikali. Kwa hiyo, gharama inabaki pale lakini Serikali inatoa mchango wake inaweza kulipia kile cha ziada ili mtumiaji aweze kupata faida.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunaendelea kuratibu hiyo na kusimamia maeneo yote ambayo tunatoa ruzuku, msamaha kuwa yanauzwa kwa bei ambayo tumekubaliana na sasa iuzwe baada ya kutoa msamaha.

Mheshimiwa Spika, ninataka niwahakikishie Watanzania tutaendelea kufatilia maeneo yote amabayo tumetoa msamaha, tutaendelea kufatilia maeneo yote tuliyotoa ruzuku ikiwemo na mbolea kama ambavyo Wizara ya Kilimo na kila kiongozi wa Serikali tunapofanya ziara kwenye Wilaya huko, tunaendelea kutoa misamaha hiyo ili kudhibiti mfumuko wa bei. Huo ndio utaratibu unatumiaka ndani ya Serikali, ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister