Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 4 2023-02-02

Name

Edward Olelekaita Kisau

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kwa kuwa viboko hivi vinaleta taharuki kubwa sana kwa nini msilete mwongozo tu aidha tukafuta kabisa ama walau kutoka nne iwe moja? Ahsante.

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Olelekaita, Mbunge wa Kiteto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Olelekaita ametoa ushauri; na kwa kuwa hii ilikuwa ni kanuni zilizokuwa zimewekwa na zikatolewa na waraka kutoka Wizara ya Elimu na Utamaduni, basi kwa ushairi huo tunauzingatia tutaona kama inawezekana, wadau watahusishwa, wataangalia mwenendo wa nidhamu, matatizo ya nidhamu yaliyopo nchini na pia wakati tulionao, ambao ndio unaowezesha. Hata sisi Wabunge kubadilisha sheria moja na kuifanyia maboresho inatokana na wakati. Kwa hiyo nalo pia tutaliangalia kama wakati unaruhusu kuondoa viboko vinne mpaka kimoja au kuondoa kabisa basi wadau watatushauri, na Serikali tupo tayari kutekeleza pale ambako inaonekana wadau watakubaliana na hilo, ahsante sana.

Additional Question(s) to Prime Minister