Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 3 2023-02-02

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Gender

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, wakati Waziri Mkuu anatoa maelezo yake amesema sasa ni marufuku watu kutoa taarifa ya matokeo haya katika social media. Matendo haya yamekuwa yakifanyika na yanafichwa na wakati mwingine viongozi wahusika wanalinda waliyoyatenda. Je, Waziri Mkuu haoni kuwa kitendo cha kuwazuia watu kutotoa taarifa ambayo ilikuwa inasaidia viongozi wahusika kuchukua hatua haraka, huoni kwamba matendo hayo yataendelea kufanyika na yataendelea kufichwa?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rwamlaza, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimeeleza kwenye taarifa yangu, kwamba malengo ya kutahadharisha kuleta mkanganyiko, taharuki kwenye jamii hayalengi kulinda maovu yanatotokea bali yanalenga katika kuifanya jamii iendelee kuwa tulivu. Kwa sababu gani; taratibu zibainishwe pale ambapo mtu anakiuka utaratibu basi hatua kali zinachukuliwa.

Mheshimiwa Spika, tunatambua tukio ambalo limejitokeza pale Kyelwa aliyechukua video ni mwalimu ambaye alishindwa kumwelekeza mwalimu mwenzake kwamba jambo hilo lisifanyike kwa sababu ni kiongozi wa juu kwa cheo. Lakini bado alikuwa ana uwezo wa kutoa taarifa kwa maafisa elimu wao wa kata, pia tuna afisa elimu wa wilaya na adhabu zikachukuliwa. Kwa hiyo video ile aliyochukua badala ya kuirusha kwenye mtandao angeweza kuipeleka pia kwa afisa elimu kama ushahidi wa tukio lililotokea mahali pa kazi.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo bado hatusisitizi sana hilo kwa sababu limesaidia pia kutoa taarifa. Hata hivyo, katika kuzuia taharuki na kutoa picha ambayo kwa jamii juu ya matendo yanayotendeka kwenye maeneo haya tulilazimika pia kushauri kwamba ni vizuri taratibu zikaenda kwenye mamlaka husika, kwa sababu mamlaka zipo na zimeainishwa kisheria pia.

Additional Question(s) to Prime Minister