Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 53 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 4 2021-06-17

Name

Grace Victor Tendega

Gender

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ya kumuuliza swali Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mamlaka za Wilaya zilizokuwa na ofisi maeneo ya mjini zilizo nyingi zilitekeleza maagizo ambayo yalitolewa na Serikali ofisi zao ziweze kuondoka pale mjini ili zipelekwe katika halmashauri zao. Na kitendo hiki kilifanya halmashauri nyingi na wananchi wengi kukosa huduma bora ambazo walizoea. Lengo la kuziacha pale mjini ilikuwa wananchi waweze kupata huduma na utawala bora kama ilivyokuwa lengo kubwa lakini kwenda kule kumeongezea kwanza umbali kwa sababu lazima wafike mjini ndio waende kule lakini pia gharama inakuwa kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unavyojua kule vijijini usafiri ni wa mabasi, mabasi yanatoka asubuhi alfajiri yanafika na yanarudi mchana kwa hiyo akikosa huduma kwa wakati anashindwa kurudi kwa hiyo inamlazimu kulala. Je, nini kauli ya Serikali ya kuwapunguzia wananchi adha hii na kuhakikisha kwamba wanapata huduma kwa gharama nafuu na kwa utawala bora uweze kutekelezeka. (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la mheshimiwa Tendega, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, anachokisema Mheshimiwa Mbunge ni agizo la Serikali la Halmashauri hasa za Wilaya ambazo zilikuwa kwenye Makao Makuu ya Wilaya zake ambapo pia waliacha wahudumiwa wako mbali na maeneo ya kutolea huduma. Mheshimiwa Rais Hayati Dkt. John Pombe Magufuli wa Awamu ya Tano alitoa maelekezo kwamba Halmashauri za Wilaya ziondoke kwenye Halmashauri za Miji walimo badala yake wajenge kwenye Halmashauri za Wilaya hukohuko ambapo wananchi walipo kwa lengo la kutoa huduma kwa urahisi ili kumuondolea gharama mwananchi aliyepo kwenye halmashauri hiyo. Kwa hiyo, lengo ilikuwa ni kumuondolea gharama mwananchi aliyepo kwenye eneo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa wapi makao makuu hiyo inajengwa ilikuwa ni maamuzi ya wananchi wenyewe kupitia wawakilishi wao Baraza la Madiwani ambalo pia lenyewe limejadili pamoja na watalaam na kuchagua maeneo ya kujenga. Baada ya uchaguzi huo, sasa ujenzi utaanza na Serikali tulikuwa tunapeleka fedha na tumepeleka fedha; tumeanza awamu ya kwanza kugawa fedha kupeleka kwenye halmashauri mpya ili wajenge Makao Makuu ya Halmashauri; tumpeleka pia awamu ya pili na tutapeleka awamu ya tatu kwa sababu bado hatujakamilisha halmashauri zote. Lakini bado kuna halmashauri ambazo pia zina miundombinu kongwe, nazo pia tunazijengea makao makuu mpya. Kwa hiyo, tutapeleka pia na fedha kwenye halmashauri kongwe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, malengo yetu ni kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma hizi kwa ukaribu kuondoa gharama uliyoisema kwa kupeleka mahali ambapo wao wamepanga na ndiko kunawarahisishia kupunguza gharama hizo, hayo ndio malengo. Sasa inawezekana pia huko wamepanga vinginevyo inawasababishia wengine kuwa na gharama kubwa lakini ni jukumu lao kupanga wapi wanaweza kujenga Halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, natambua yapo maeneo ambayo jiografia yake haiwezekani; Wilaya kama Uyui tulipata shida sana tulipoamua wajenge makao makuu maeneo yalipo sasa kwa sababu Halmashauri ya Uyui iko kama yai imezunguka Manispaa ya Tabora. Kwa hiyo, mtu anayetoka huku lazima apite Makao Makuu ya Mji ili aende kwenye Makao Makuu mpya. Zipo halmashauri jiografia yake ni ngumu lakini lazima tuanze mahali halafu tuende mahali vizuri. Kwa hiyo, tutaendelea kusikiliza maeneo yote yenye jiografia ngumu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na hivi karibuni nilikuwa Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma, nilikuta hiyo, Halmashauri ya Mbinga Vijijini ambayo Mheshimiwa Mbunge hapa yupo ramani/jiografia yake ni ngumu kidogo, popote utakapoweka Makao Makuu ya halmashauri, lazima kutakuwa na mgogoro lakini bado tunapokea changamoto hiyo na tutaifanyia kazi. Malengo ni kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma hizo ili iwarahisishie katika kutoa huduma na wananchi wapate huduma kwa ukaribu kwa gharama nafuu, hayo ndio majibu ambayo kwa sasa Serikali inayafanyia kazi. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister