Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 33 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2019-05-23

Name

Esther Nicholus Matiko

Gender

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Mheshimiwa Waziri Mkuu ni wajibu wa Serikali kuyahudumia majeshi yetu kwa kuyapatia uniform ambazo ni viatu, soksi, suruali au sketi, shati, mkanda wa suruali, mkanda wa filimbi, nembo ya cheo, lakini na kofia. Imekuwa ni muda mrefu sasa majeshi haya hayapatiwi hizi uniform badala yake wanajinunulia wao wenyewe.

Mheshimiwa Spika, mathalani Jeshi la Magereza tangu 2012 hawajawahi kupatiwa uniform, vivyohivyo kwa Jeshi la Polisi na hizi uniform wanajinunulia kwa bei ghali sana. Mathalani nguo ambazo za jungle green wananunua kwa 70,000/=, kofia 15,000/=, buti zile 70,000/= na hawa askari wetu wanafanya kazi kwa mazingira magumu sana.

Mheshimiwa Spika, ningetaka kujua sasa ukizingatia Askari Magereza kwa mfano mwenye degree analipwa sawa na Askari Magereza mwenye elimu ya kidato cha nne, shilingi 400,000 aweze kununua, ajigharamie nyumba na mambo mengine.

Ni nini sasa Kauli yako Mheshimiwa Waziri Mkuu kuhakikisha kwamba, askari hawa wanapewa uniform zao, maana ni stahiki ambayo wanatakiwa kupewa, sanjari na kurudishiwa gharama zote ambazo wamekuwa wakijinunulia hizi uniform kwa kipindi chote ambacho Serikali ilishindwa kuwapa hizi uniform?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Tarime, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kimsingi Serikali inao wajibu wa kutoa vifaa mbalimbali ikiwemo sare kwa majeshi yetu, ili waweze kufanya kazi yao kwa urahisi zaidi. Wizara ya Mambo ya Ndani ambayo inasimamia Jeshi la Polisi, Magereza pamoja na Uhamiaji pamoja na Zimamoto ni Wizara ambayo inaendelea kuratibu namna nzuri ya kupata sare na vifaa mbalimbali, ili kuwawezesha watumishi wetu askari kwenye majeshi hayo waweze kufanya kazi yao. Na sera yetu ni kwamba, bado Serikali itaendelea kuwagharamia.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ni shahidi mwaka jana tumekuwa tukijadili upande wa Jeshi la Polisi, Wizara ya Mambo ya Ndani ilipokuwa imeagiza, imetoa zabuni ya kununua sare na tukapata taarifa kwamba, kuna majora yako pale ambayo yameandaliwa kwa ajili ya kuwapa askari, hiyo ni dalili kwamba, Wizara ya Mambo ya Ndani bado inatoa huduma hizo kwa askari wake.

Mheshimiwa Spika, sasa kama kuna mahali ambako kwa Wizara upande huo wananunua hizo sare tutaweza kuwasilisna pia na Waziri mwenye dhamana, ili tuone kwa utaratibu huo ukoje na kwa nini sasa askari wanunue na kama ndio sera ya ndani ya Wizara tutaweza kujua na tunaweza tukafanya marekebisho kadiri ya mahitaji yalivyo, ahsante.

Additional Question(s) to Prime Minister

Name

Esther Nicholus Matiko

Gender

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nakushukuru Waziri Mkuu. Mheshimiwa Waziri Mkuu ni ukweli kabisa kwamba, hawa askari hawapewi hizi sare na hata wakifanya parade utaona uniform zao ziko tofauti-tofauti kwa texture, lakini hata kwa rangi.

Mheshimiwa Spika, nilitaka pia kujua, maana hujajibu swali langu lile jingine, fidia ambazo watarudishiwa gharama ambazo wakati mnaendelea kujiratibu kuhakikisha wanapewa hizi uniform. Je, wataweza kuridishiwa gharama ambazo wamekuwa wakizitumia kujinunulia uniform zao wenyewe?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sasa kwa sababu umelieleza hilo na unaonesha unazungumza kama una uhakika wa kwamba, askari wetu wananunua. Na ungependa kujua je, kama askari hao wanaweza kurudishiwa fedha zao kama sera ya kuwapa vifaa bure ipo?

Mheshimiwa Spika, basi naomba nilichukue hilo niwasiliane na Wizara husika, ili tuone msingi wa ununuzi wa vifaa hivyo, halafu tutaweza kuzungumza vizuri na Wizara ya Mambo ya Ndani na tutakupa taarifa Mheshimiwa Mbunge, ahsante. (Makofi)