Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 34 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 1 2019-05-23

Name

Asha Abdullah Juma

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Spika, asante sana. Nashukuru sana kupata fursa hii ya kipekee na ya heshima kubwa sana kwangu na kwa Serikali yangu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu, utendaji na utekelezaji wa Ilani ya chetu cha CCM kwa kiasi kikubwa umekuwa na mafanikio. Mheshimiwa Waziri Mkuu utekelezaji wa ilani katika sekta ya kilimo, nishati, elimu, afya, madini, n.k. kumekuwa na hatua ya kuridhisha sana.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa karibu kipindi chetu kinakwisha tunakaribia uchaguzi Mkuu wa 2020 naomba kuuliza Serikali, lakini kabla sijauliza niseme kwamba, mafanikio haya tuliyoyafikia leo yamefikiwa kupitia na juhudi kubwa za Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na timu yake akiwemo Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mheshimiwa Samia, Waziri Mkuu wewe mwenyewe Majaliwa na watendaji wote wa Serikali ambao wamefanya kazi nzuri kufikia maeneo hayo niliyoyataja hapo juu. Sasa hivi Serikali itakamilisha lini utaratibu wa kuwawezesha Watanzania wanaoishi nchi za nje kuweza kupata nafasi yao ya kidemokrasia kupiga kura?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asha, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa anataka kujua Serikali inaandaa utaratibu upi wa kuwezesha Watanzania walioko nje ya nchi kuja kupiga kura nchini wakati wa uchaguzi mkuu na chaguzi nyingine:-

Mheshimiwa Spika, jambo hili ni la kisera na Serikali imeendelea kuona utaratibu huo kama unaweza kufaa kwa sababu, lazima kwanza tupate kujua nani wako nje ya nchi, idadi yao, wanafanya shughuli gani na kama je, bado ni Watanzania au waliomba uraia nchi za nje. Na pindi sera hiyo itakapokamilika pale ambapo itaonekana inafaa tutakuja kulijulisha wote, Bunge na Tanzania nzima. Asante sana.

Additional Question(s) to Prime Minister