Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 8 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 5 2019-09-12

Name

Julius Kalanga Laizer

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimia Spika, nakushukuru. Mwaka huu maeneo mengi ya nchi yetu yamekabiliwa na upungufu wa mvua ambayo imepelekea maeneo mengi kukosa chakula cha uhakika na hivyo kusababisha bei ya chakula kupanda kwa kiasi kikubwa sana. Hapa tunapozungumza maeneo mengi mahindi yanauzwa kuanzia shilingi elfu 80 mpaka laki moja.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu, je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba chakula cha bei nafuu kutoka NFRA kinapelekwa katika maeneo haya yaliyokumbwa na ukame ili wananchi waweze kumudu chakula? (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kalanga, Mbunge wa Monduli kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, uzalishaji wa chakula nchini kwa maana usalama wa chakula nchini kufuatia msimu uliopita wa uvunaji wa mazoa ya chakula uko vizuri, lakini tunatambua kwamba yako maeneo kadhaa hali ya hewa haikuwa nzuri na uzalishaji wake haukuwa mzuri sana. Kwa hiyo, maeneo hayo yanaweza kuathirika kwa kuwa na bei zisizotabirika wakati wote na kusababisha wananchi kutojua hasa bei ya mahindi, chakula hicho, lakini pia ni wapi tunaweza kupata chakula hicho.

Mheshimiwa Spika, lakini nataka niwahakikishie kwamba uzalishaji wa chakula ambao umefanywa, ambao Wizara ya Kilimo imeweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba maeneo yote yanapata chakula, NFRA imepewa jukumu la kuhakikisha kwamba usalama wa chakula nchini unaimarishwa kwa kuwa na chakula cha akiba kwenye maghala ili kiweze kutolewa na kuuzwa kwenye maeneo ambayo hayana chakula kwa sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pili, kwa kuwa chakula kiko nchini na tunao wafanyabiashara ndani ya nchi, hiyo ni fusa muhimu kwao ya kupata chakula kukipeleka maeneo ambayo hayana chakula. Mheshimiwa Kalanga amezungumzia bei nafuu, bei nafuu sasa ni tumeruhusi wanunuzi mbalimbali kuingia kununua. Wanapokuwa wanunuzi wengi kunakuwa na ushindani wa ununuzi, ingawa pia bei inakuwa iko juu lakini sisi kwa sababu tuna NFRA ambayo inashughulikia usalama wa chakula, basi chakula huwa kinapatikana. Kwa hiyo, muhimu zaidi tupate taarifa, wapi kuna upungufu wa chakula, halafu tuone, tuweze kupeleka chakula ambacho tunaweza kununua kwa bei nafuu.

Mheshimiwa Spika, lakini muhimu zaidi ni ule msisitizo wa kila mmoja afanye kazi na tumeanza kuona matunda kwamba chakula sasa uzalishaji ni mkubwa mpaka tunakua na ziada hapa nchini na chakula kingine tunauza pia hata nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, lakini mbili, ni hilo ambalo tumelisema la kwamba wanunuzi sasa wapite maeneo hayo waweze kuchukua mahindi kutoka eneo moja kupeleka eneo la pili ili wananchi wa maeneo hayo waweze kupata huduma.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kupitia Mheshimiwa Kalanga NFRA inaweza ikipata taarifa na Wizara ya Kilimo inasikia hapa ni rahisi sasa kuweza kushughulikia maeneo hayo yanayokosa chakula. Kwa hiyo, kwa taarifa ambayo tumeipata sasa naamini tutaishughulikia ili kuona namna nzuri ya kufikisha chakula ambacho tunaweza kukinunua kwa bei nafuu. Ahsante.

Additional Question(s) to Prime Minister