Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 9 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 5 2019-02-07

Name

Silafu Jumbe Maufi

Gender

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, napenda kutoa shukrani ya dhati kwa kunipatia fursa hii ili niweze kumuuliza Mheshimiwa Waziri Mkuu swali.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na hali ya kusuasua katika utekelezaji wa Miradi ya REA kufikisha umeme vijijini. Hivi Serikali imejipanga vipi kuhakikisha kwamba miradi hii sasa inakwenda kwa kasi ili wananchi wa vijijini waweze kupata umeme, kwani umeme ni maendeleo? Naomba jinsi Serikali ilivyojipanga na kuhakikisha kwamba sasa Miradi hii ya REA itakwenda vizuri katika nchi yetu. (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tuna Miradi ya REA na inatekelezwa nchi nzima. Wizara ya Nishati kupitia TANESCO ilishapata wakandarasi na imewasambaza wanafanya kazi hizo maeneo yote. Malengo ya Serikali ni kuhakikisha kwamba miradi hii inatekelezwa kila eneo kadri tulivyokubaliana na mikataba na wale wakandarasi wanaofanya kazi hiyo. Pia sisi na Mheshimiwa Waziri tunapopita huko tunafuatlia mwenendo wa utekelezaji wa miradi hiyo ili tujiridhishe vijiji vyote vilivyoingia kwenye orodha viweze kupata umeme kadri tulivyokubaliana na wakandarasi wetu.

Mheshimiwa Spika, lakini tutambue kwamba hapa katikati kulikuwa na migogoro kidogo kati ya wazalishaji nguzo na wamiliki wa mashamba yanayozalisha nguzo ambapo walikuwa wanatofautiana kuhusu kodi. Jambo hili nilipolipata mezani kwangu nililifanyia kazi kwa kuita mamlaka zote ili kupata maelezo ya msingi ili kuhakikisha kwamba kazi hii inaendelea. Nashukuru sana Mikoa ya Iringa na Njombe pamoja na na Wilaya zote kwamba tatizo walilokuwa wanabishana nalo la ulipaji kodi ambalo hasa lilikuwa linagusa kwenye tafsiri ya sheria lilikwisha na kazi inaendelea vizuri, wazalishaji nguzo wanaendelea kuzalisha nguzo na wale wakandarasi wanaendelea kupelekewa nguzo kwenye maeneo yao na kazi inaendelea vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge wenzangu na hasa Mheshimiwa Mbunge uliyetaka majibu na Watanzania wote kwenye vijiji ambavyo vimewekwa kwenye mpango kwa ajili ya kupelekewa umeme, tutahakikisha unakwenda kwenye maeneo yote. Serikali inayo fedha kuwalipa wakandarasi, wakandarasi nao wanawajibika kutekeleza kwa mujibu wa mikataba na wale wote ambao tumesaini mikataba ya kuzalisha nguzo waendelee na kazi hiyo, pale ambako wanatakiwa kutekeleza masharti maeneo wanayozalisha nguzo wafanye hivyo kwa sababu uzalishaji huo na malipo yote ni ya kisheria. Kwa kuwa wameendelea kutekeleza jambo hili tumemuachia kazi Mkuu wa Mkoa wa Iringa kuhakikisha kuwa wazalishaji wanaendelea vizuri na kazi yao na wakandarasi wanaoingia kwenye Wilaya hizo wanapewa mizigo yao na wanasafiri kwenda kwenye maeneo yote ili kazi iweze kuendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, zoezi la usambazaji umeme linaendelea na kama kuna tatizo la kusuasua huko Waheshimiwa Wabunge mtupe taarifa ili Mheshimiwa Waziri na yeyote mwenye dhamana anaweza kwenda kuona tatizo liko wapi ili tutatue tatizo hilo. Malengo ya Serikali ni kuhakikisha kwamba tunapata umeme maeneo yote ili Watanzania mpaka kwenye ngazi ya vijiji, kama ambavyo mmsesikia sasa uwekaji wa umeme tunaweka kwenye nyumba zote ya bati, isiyokuwa ya bati ili Watanzania wapate mwanga. Malengo yetu tunaamini yatakamilika na pale ambako kutakuwa na tatizo tutashughulikia. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge uwe na amani. Ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister