Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 8 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2017-11-16

Name

Catherine Nyakao Ruge

Gender

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ili na mimi niweze kuuliza swali.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, Sera ya Elimu ya Mwaka 2014 inatamka wazi kuwezesha mazingira bora kwa wanafunzi wote kwa maana ya wanafunzi wa kike na wa kiume bila kujali jinsia. Hata hivyo, kuna utafuti uliofanywa na Tanzania Gender Network Program, unaonesha kwamba watoto wa kike hukosa masomo kati ya siku tatu mpaka saba kwa mwezi na hivyo huathiri ufaulu wao. Ni kwa nini sasa Serikali haioni umuhimu wa kutoa mwongozo kwa zile pesa za ruzuku zinazokwenda shuleni kutamka wazi kwamba kiasi fulani kitengwe kwa ajili ya taulo za kike ili watoto hawa waweze kuhudhuria masomo siku zote?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ruge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kweli tunayo Sera ya Elimu na sera yetu tunasisitiza watoto wote wa Kitanzania wasome (wa kiume na wa kike) na tunaendelea kusimamia uwepo wa idadi kwa idadi kwanza iwe idadi nzuri ya wasichana na wavulana kwenye elimu.

Mheshimiwa Spika, sasa yako haya mambo ya ndani ambayo tunaingiza zaidi kwenye Sekta ya Afya na Wizara ya Afya ambayo pia inalishughulikia hili kwa ujumla wake nayo pia tumeipa jukumu la kuratibu shughuli zote zinazohusu afya. Hata hivyo, kwenye shule zetu hatukuweza kuitamka hiyo wazi kwa sababu tunaamini kwamba mwanafunzi anapopata tatizo hilo haliwezi kuwa public, ni jambo binafsi.

Mheshimiwa Spika,Sasa mambo hayo binafsi ingawa yanaweza kuathiri kipindi cha masomo lakini tunaamini kwamba tunaweza tukawa tunawatunza watoto wetu pamoja na ndiyo sababu katika kila shule tumeamua kuwe na Walimu wanawake ili waweze kumsaidia mtoto wa kike kwa hayo mambo ambayo ni ya ndani, ya usiri, hatuwezi kuyaweka wazi. Pale ambapo tutaona kuna umuhimu zaidi wa kuhakikisha kwamba tunaweza kuandaa sera ya namna hiyo kwa ajili ya kuwakinga akinamama, tunaweza kufanya hilo.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Matrons wetu walioko shuleni wanaendelea kukaa nao watoto wetu ili kumfanya nae pia kuendelea kuwa na confidence ya kusoma pamoja na wenzake bila kuibua hizo hisia ambazo tunasema ni mambo ya usiri na ya ndani ingawa pia ni muhimu nalo katika kuliweka kwenye utaratibu huo ambao tunadhani ni muhimu pia kuufanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kwa swali la Mheshimiwa Mbunge, ni suala muhimu lakini linazungumzika ndani ya Serikali ili tuweze kulifanyia kazi.

Additional Question(s) to Prime Minister