Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Questions to the Prime Minister from Hon. Richard Phillip Mbogo (3 total)

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, ina sera nzuri, ina sheria mbalimbali juu ya elimu ambazo zinapelekea wanafunzi wa Kidato cha Nne waliofaulu, wanachaguliwa na kwenda Kidato cha Tano. Mara nyingi kwa maarufu wamesema huwa kunakuwa na selection.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kuna habari ambazo zinazagaa kwamba mwaka huu Serikali haitachukua wanafunzi kutokana na sababu ambazo bado hazijaeleweka. Sasa je, Mheshimiwa Waziri Mkuu, jambo hili lina ukweli gani? Kama lipo, Serikali inatoa kauli gani juu ya suala hilo?
imiwa Mbogo, Mbunge wa Nsimbo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nataka nikanushe kwamba Serikali haina mpango wa kuwapanga vijana wetu waliomaliza Kidato cha Nne kwenda Kidato cha Tano. Najua tuna makundi mengi ya watu wanapenda kupotosha tu habari, ikiwemo na hii, lakini nataka nitumie nafasi hii kuwahakikishia wanafunzi wote waliomaliza Kidato cha Nne, wanaopaswa kwenda Kidato cha Tano, lakini na wazazi pia wa vijana wetu hawa kwamba Wizara ya TAMISEMI yenye dhamana na Sekondari, kwa pamoja na Wizara ya Elimu, kazi ya upangaji wa vijana wanaokwenda Kidato cha Tano inaendelea na wakati wowote ule mwishoni mwa mwezi huu majina hayo yatakuwa yametoka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zinazofanywa sasa, nyie wote mnatambua kwamba mwaka uliopita wanafunzi hawa walikuwa wanapangwa kwa mfumo wa GPA na sasa tumebadilisha GPA kwenda division. Kwa hiyo, kazi ambayo Wizara ilikuwa inafanya ni kubadilisha ule mfumo wa GPA kwenda division ili uweze kuwapanga vizuri kwa division zao na sifa ambazo zinatakiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la upangaji halikuwa ni kwa ajili ya Kidato cha Tano peke yake, kuna wale ambao tunawapeleka Vyuo kama Afya, Kilimo na maeneo mengine, nao pia wanatakiwa wapangwe kwa mfumo wa division na wote hao unapowapanga Kidato cha Tano, ili wengine waweze kupangwa, zoezi hili lazima lifanywe kwa pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kazi hii inakamilika, itatoka muda mfupi ujao na kwa hiyo, baada ya hapo Serikali itatoa majibu haya wiki mbili kabla ili kuwawezesha wazazi kujipanga vizuri kuwapeleka vijana wao kwenye maeneo mengine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kulikuwa na kazi ya sensa ya kuhakikisha tuna shule ngapi za Kidato cha Tano ili tuweze kuwapeleka vijana wetu wote. Kwa sababu mwaka huu ufaulu ni mkubwa zaidi, kuliko mwaka jana, 2015. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, lazima tuhakikishe tunawapeleka vijana kulingana na uwezo wa shule ili tujue tumewapeleka wangapi na wanaobaki wangapi wenye stahili ya kwenda Kidato cha Tano ili nao wapate nafasi ya kupangiwa maeneo mengine kwa stahili ile ile ya Kidato cha Tano ili waziweze kupoteza ile stahili yao waliyokuwanayo ya Kidato cha Tano; kama vile kuwapeleka kwenye course za miaka mitatu za Diploma ambapo miaka miwili huitumia kwa ngazi ya Kidato cha Tano na cha Sita, wakishafaulu wanaingia kwa profession, kama ni afya, kama ni kilimo, kama ni sekta nyingine; kwa mfano Ualimu, ili waweze kuendelea na stahili yao ya Kidato cha Sita. Kwa hiyo, kazi hiyo itakapokamilika, tutaweza kutoa taarifa mapema.
MHE. RICHARD P. MBOGO:
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, ina sera nzuri, ina sheria mbalimbali juu ya elimu ambazo zinapelekea wanafunzi wa Kidato cha Nne waliofaulu, wanachaguliwa na kwenda Kidato cha Tano. Mara nyingi kwa maarufu
wamesema huwa kunakuwa na selection.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kuna habari ambazo zinazagaa kwamba mwaka huu Serikali haitachukua wanafunzi kutokana na sababu ambazo bado hazijaeleweka. Sasa je, Mheshimiwa Waziri Mkuu, jambo hili lina ukweli gani? Kama lipo, Serikali inatoa kauli gani juu ya suala hilo?
WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbogo, Mbunge wa Nsimbo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nataka nikanushe kwamba Serikali haina mpango wa kuwapanga vijana wetu waliomaliza Kidato cha Nne kwenda Kidato cha Tano. Najua tuna makundi mengi ya watu wanapenda kupotosha tu habari, ikiwemo na hii, lakin
i nataka nitumie nafasi hii kuwahakikishia wanafunzi wote waliomaliza Kidato cha Nne, wanaopaswa kwenda Kidato cha Tano, lakini na wazazi pia wa vijana wetu hawa kwamba Wizara ya TAMISEMI yenye dhamana na Sekondari, kwa pamoja na Wizara ya
Elimu, kazi ya upangaji wa vijana wanaokwenda Kidato cha Tano inaendelea na wakati wowote ule mwishoni mwa mwezi huu majina hayo yatakuwa yametoka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zinazofanywa sasa, nyie wote mnatambua kwamba mwaka uliopita wanafunzi hawa walikuwa wanapangwa kwa mfumo wa GPA na sasa tumebadilisha
GPA kwenda division. Kwa hiyo, kazi ambayo Wizara ilikuwa inafanya ni kubadilisha ule mfumo wa GPA kwenda division ili uweze kuwapanga vizuri kwa division zao na sifa ambazo zinatakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la upangaji halikuwa ni kwa ajili ya Kidato cha Tano peke yake, kuna wale ambao tunawapeleka Vyuo kama Afya, Kilimo na maeneo mengine, nao pia wanatakiwa wapangwe kwa mfumo wa division na wote hao unapowapanga Kidato cha Tano, ili wengine waweze kupangwa, zoezi hili lazima lifanywe kwa pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kazi hii inakamilika, itatoka muda mfupi ujao na kwa hiyo, baada ya hapo Serikali itatoa majibu haya wiki mbili kabla ili kuwawezesha wazazi kujipanga vizuri kuwapeleka vijana wao kwenye maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kulikuwa na kazi ya sensa ya kuhakikisha tuna shule ngapi za Kidato cha Tano ili tuweze kuwapeleka vijana wetu wote.
Kwa sababu mwaka huu ufaulu ni mkubwa zaidi, kuliko mwaka jana, 2015.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, lazima tuhakikishe tunawapeleka vijana kulingana na uwezo wa shule ili tujue tumewapeleka wangapi na wanaobaki wangapi wenye stahili ya kwenda Kidato cha Tano ili nao wapate nafasi ya kupangiwa maeneo mengine kwa stahili ile ile ya Kidato cha Tano ili waziweze kupoteza ile stahili yao waliyokuwanayo ya Kidato cha Tano; kama vile kuwapeleka kwenye course za miaka mitatu za Diploma ambapo miaka miwili huitumia kwa ngazi ya Kidato cha Tano na cha Sita, wakishafaulu
wanaingia kwa profession, kama ni afya, kama ni kilimo, kama ni sekta nyingine; kwa mfano Ualimu, ili waweze kuendelea na stahili yao ya Kidato cha Sita. Kwa hiyo, kazi hiyo itakapokamilika, tutaweza kutoa taarifa mapema.
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa usikivu wake ilisikia kilio ambacho Wabunge pamoja na wananchi kuhusiana na migogoro ya ardhi ambayo imehusisha vijiji zaidi ya 360 katika muingiliano wa mipaka kati ya vijiji pamoja hifadhi za taifa au hifadhi za misitu au hifadhi za misitu au mapori tengefu n kupelekea hivyo Mheshimiwa Rais aliunda kamati ya Mawaziri nane wakiongozwa na Mheshimiwa Lukuvi katika kuratibu na kumshauri namna bora ya kutatua changamoto hii ya vijiji hivi zaidi ya 360, vikiwemo Vijiji vya Mataweni na Stalike katika Jimbo la Nsimbo.

Mheshimiwa Spika, ningependa kujua, je, Serikali ipo tayari kukaa kwa pamoja na Wabunge kupitia taarifa hiyo ikiwa ni namna ya kufanya reconciliation ili kusiwe na malalamiko tena ya baadaye kwa sababu hili ni zoezi ambalo litakuwa linatatua kwa muda mrefu. Je, Serikali ipo tayari kukaa na Wabunge kupitia kabla ya kumkabidhi Mheshimiwa Rais ripoti hiyo?
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbogo, Mbunge wa Nsimbo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge anataka kujua kama ripoti ya ukaguzi wa ardhi ya Tume iliyoundwa na Mheshimiwa Rais kama inaweza kuja kushirikisha Wabunge hapa.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tumekuwa tukipata taarifa mbalimbali za migogoro ya ardhi kwenye maeneo kadhaa. Wizara ya Ardhi imefanya kazi nzuri ya kupita maeneo yote yenye migogoro ya ardhi na mwisho Mheshimiwa Rais aliunda timu ya Mawaziri wanane kupita maeneo yote yenye migogoro kukagua na kusikiliza maoni ya wananchi kwenye maeneo hayo ili kuweza kuratibu vizuri na hatimaye tuweze kutoa utatuzi wa migogoro hiyo. Sasa timu ile ni ya Mheshimiwa Rais, matokeo ya ukaguzi wake yatawasilishwa kwa Mheshimiwa Rais kwanza kabla ya kupelekwa mahali pengine, kiitifaki inatakiwa iwe hivyo.

Mheshimiwa Spika, lakini pia timu ile ilipokuwa inapita kwenye maeneo yale, tuliwaagiza Mawaziri watoe taarifa kwenye Mamlaka za Wilaya kule ili watu/wadau wote washirikishwe kule, tuna amini kama kulikuwa na Wabunge na wakati ule ulikuwa siyo wakati wa Bunge, mliweza kushiriki kwa namna moja au nyingine. Pia Mheshimiwa Rais ikimpendeza, baada ya kupata taarifa hiyo, anaweza kutujulisha lakini sasa kiitifaki kwanza aliyetaka tume iundwe ndiye ambaye ambaye tunaweza kumpelekea kwanza, hatuwezi kuileta Bungeni kwanza bila kumpelekea Mheshimiwa Rais mwenyewe kiitifaki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hilo litaangaliwa na kama Mheshimiwa Rais itampendeza anaweza akaamua kutushirikisha lakini tuna amini Wabunge kwa taarifa tulizopeleka kule kwenye halmashauri zenu ili muweze kushiriki katika kutambua na kusaidia kueleza migogoro na kama ambavyo mmekuwa mkieleza hapa ndani, yale maoni yenu ya hapa ndani ndiyo yaliyochukuliwa na kwenda kuyafanyia kazi, ahsante sana. (Makofi)