Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Bonnah Ladislaus Kamoli (23 total)

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika Jimbo la Segerea kuna zahanati kumi lakini hakuna zahanati moja iliyopandishwa hadhi kuwa kituo kikubwa cha afya chenye uwezo wa kulaza wagonjwa.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuipandisha hadhi Zahanati ya Tabata „A‟ kuwa Kituo cha Afya kwa sababu ina miundombinu yote inayofaa kwa Kituo cha Afya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kabla sijajibu swali naomba nifanye correction ya data, kulikuwa kuna typing error hiyo mwaka 2015/2016 isomeke 2016/2017.
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Kaluwa, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, zahanati ya Tabata „A‟ haina eneo la kutosha kukidhi upanuzi wa miundombinu unaohitajika na hivyo inakosa sifa ya kupandishwa hadhi kuwa Kituo cha Afya. Ili zahanati iweze kupandishwa hadhi kuwa Kituo cha Afya inatakiwa kuwa na wodi ya wanaume na wanawake zenye vitanda 24 kila moja, jengo la upasuaji, jengo la wagonjwa wa nje (OPD), huduma za mama na mtoto, chumba cha kuhifadhia maiti na kichomea taka incinerator.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa zahanati ya Segerea ina eneo la kutosha, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imetenga shilingi milioni 75. katika bajeti ya mwaka 2016/2017 ili kujenga wodi zinazotakiwa ikiwa ni maandalizi ya kuipandisha hadhi Kituo cha Afya. Taratibu za kupandisha hadhi zahanati kuwa Kituo cha Afya zinaanza katika Halmashauri yenyewe kupitia vikao vyake, hatimaye maombi hayo yatawasilishwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ili kuipatia kibali.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Mwaka 1995 Serikali ilifanya uthamini wa wananchi wa Kata ya Kipawa ili kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege Dar es Salaam ambapo baadhi ya wananchi hao walilipwa fidia lakini kuna baadhi ambao mpaka sasa bado hawajalipwa fidia hiyo na hawajui ni lini watalipwa:-
Je, Serikali imejipanga vipi kuwalipa wananchi hao ambao hawajalipwa ili waweze kupisha upanuzi wa uwanja?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonna Mosses Kaluwa, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali ilifanya uthamini wa mali za wananchi ili kupisha upanuzi wa kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Dar es Salaam mwishoni mwa miaka ya 90. Maeneo yaliyoainishwa kwa ajili ya upanuzi huo ni Kipawa, Kigilagila na Kipunguni. Kutokana na ufinyu wa bajeti, Serikali imekuwa ikilipa fidia wakazi hao kwa awamu kama ifuatavyo:-
(a) Mwaka 2009/2010: Kaya/wakazi wapatao 1,500 wa eneo la Kipawa walilipwa fidia zilizofikia shilingi za Kitanzania bilioni 18. Zoezi hili lilikamilika Januari, 2010.
(b) Katika mwaka wa fedha 2010/2011, Serikali ililipa shilingi za Kitanzania bilioni 12 za fidia kwa wakazi 864 wa eneo la Kigilagila na malipo yalikamilika Januari 2011.
(c) Mwaka 2013/2014 Serikali ililipa shilingi za Kitanzania bilioni 1.2 ikiwa ni fidia kwa wakazi 59 kati ya wakazi 801 wa eneo la Kipunguni.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, hadi sasa ni wakazi wapato 742 wa Kipunguni ndio ambao hawajalipwa fidia zao yenye thamani ya takriban shilingi bilioni 19. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha fidia za wakazi hao waliosalia.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Mwaka 1995 Serikali ilifanya uthamini wa wananchi wa Kata ya Kipawa ili kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Dar es Salaam ambapo baadhi ya wananchi hao walilipwa fidia lakini kuna baadhi ambao mpaka sasa bado hawajalipwa fidia hiyo na hawajui ni lini watalipwa.
Je, Serikali imejipanga vipi kuwalipa wananchi hao ambao hawajalipwa ili waweze kupisha upanuzi wa uwanja?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali ilifanya uthamini wa mali za wananchi ili kupisha upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa Dar es Salaam mwishoni mwa miaka ya 1990. Maeneo yaliyoainishwa kwa ajili ya upanuzi huo ni Kipawa, Kigilagila na Kipunguni. Kutokana na gharama za fidia na uhaba wa fedha, Serikali imekuwa ikilipa fidia kwa wakazi hao kwa awamu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya kwanza ililipwa mwaka 2009/2010 kwa wakazi wapatao 1,500 wa eneo la Kipawa ambao walilipwa fidia zilizofikia shilingi bilioni 18 na zoezi hili lilikamilika Januari, 2010. Katika mwaka wa fedha 2010/2011, Serikali ililipa shilingi bilioni 12 za fidia kwa wakazi 864 wa eneo la Kigilagila na malipo yalikamilika Januari, 2011. Mwaka 2013/2014 Serikali ililipa shilingi bilioni 1.2 ikiwa ni fidia kwa wakazi 59 kati ya wakazi 801 wa eneo la Kipunguni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa ni wakazi 742 wa Kipunguni ndio ambao hawajalipwa fidia zao zenye thamani ya takriban shilingi bilioni 19. Katika mwaka wa fedha 2016/ 2017, Serikali ilitenga shilingi bilioni tano kwa ajili ya kulipa fidia wananchi wa Kipunguni. Aidha, katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imetenga shilingi bilioni 30 ili kukamilisha malipo ya fidia kwa wananchi hao.
MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y MHE. BONNAH M. KALUWA) aliuliza:-
Katika Jimbo la Segerea zipo shule kumi na moja za sekondari za Serikali ambapo wanafunzi wa shule hizo wanafaulu vizuri kwa kupata daraja la I, II na III na kuwa na sifa ya kujiunga kidato cha tano. Kwa mfano mwaka 2015 wanafunzi zaidi ya 400 walifaulu kwenda kidato cha tano, lakini katika Jimbo la Segerea hakuna hata shule moja ya kidato cha tano licha ya kuwa na maeneo ya kujenga ya kutosha katika shule za sekondari za Kinyerezi, Magoza na Ilala.
Je, Serikali ina mpango gani madhubuti wa kuanzisha shule za kidato cha tano na sita katika maeneo ya shule zilizotajwa ili kuwapunguzia wanafunzi hao adha ya usafiri wanayopata kwa kufuata shule mbali?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ina jumla ya shule za sekondari za Serikali 49 zikiwemo shule sita kongwe. Kati ya shule hizo, saba ni za kidato cha tano na sita. Halmashauri inaendelea kuboresha miundombinu ya shule ya sekondari Juhudi ili iwe na Kidato cha tano na sita. Aidha, katika mpango wa muda mrefu Halmashauri imepanga kuanzisha shule sita za kidato cha tano na sita kuanzia mwaka 2017 hadi 2022. Mpango wa Serikali ni kuhakikisha shule hizo zinakuwepo katika kila tarafa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za kidato cha tano na sita ni za kitaifa ambapo zinachukua wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali nchini, ndiyo maana wanafunzi 400 kutoka Jimbo la Segerea wamechaguliwa kwenda shule mbalimbali nchini.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-

Wananchi wa Kata za Kinyerezi, Bonyokwa, Segerea Liwiti, Kipawa, Kimanga, Kisukulu na Tabata wamekuwa wakitumia fedha na muda mwingi kwenda kutafuta bidhaa na huduma katika masoko ya Buguruni na Kariakoo kutokana na kukosa huduma hizo katika maeneo yao:-

(a) Je, kwa nini Serikali isijenge soko kubwa katika eneo mbadala lililo katikati na linaloweza kufikiwa na wananchi hao kwa wakati?

(b) Je, kwa nini Soko la Kinyerezi lililozinduliwa na Mwenge mwaka 2017 lisifunguliwe ili kutoa huduma kwa wananchi wanaozunguka soko hilo na maeneo ya karibu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Kamoli, Mbunge wa Segerea, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala iliweka kipaumbele cha kutekeleza mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Soko la Kisutu utakaogharimu takribani shilingi bilioni 12.17. Mpaka sasa mradi huo umepatiwa jumla ya shilingi bilioni 3.92 na ujenzi unaendelea. Aidha, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imetenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya kujenga masoko mengine ndani ya Manispaa ya Ilala. Halmashauri inashauriwa kutumia fursa ya miradi ya kimkakati na kuandaa andiko la mradi wa kujenga masoko katika Kata ya Kinyerezi, Bonyokwa, Segerea, Liwiti Kipawa, Kimanga, Kisukulu na Tabata ili kupata fedha za utekelezaji.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Soko la Kinyerezi lililozinduliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2017 limepangwa kuanza kutumika Mei, 2019 baada ya matengenezo ya choo ambacho kilikuwa hakijakamilika kwa wakati huo.
MHE. MARIAM N. KISANGI (K.n.y. MHE. BONNAH M. KALUWA) aliuliza:-

Barabara ya Segerea Sheli kupitia Seminari, Stakishari Polisi kwenda kutokea Majumba Sita ni suluhisho la Msongamano wa magari yanayopita barabara ya Segerea - Tabata kutokea barabara ya Mandela, lakini kwa sasa barabara hiyo haipitiki kwa kuwa daraja la Seminari liliondoshwa na maji ya mvua mwaka 2013.

Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kujenga daraja la Seminari ili kuondoa tatizo hilo na kurahisisha huduma kwa wananchi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba nijibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, daraja la Seminari Segerea liko katika barabara ya Majumba Sita Stakishari yenye urefu wa kilomita 2.93. Hapo awali usanifu wa kujenga daraja hili ulishafanyika. Hata hivyo, ipo changamoto inayotokana na mto kutanuka, hivyo inahitajika kufanyika stadi ya kina na mapitio ya usanifu wa awali ili kupata mahitaji halisi ya ujenzi wa daraja kutokana na changamoto hiyo. Mara baada ya kukamilika kwa mapitio ya usanifu na tathmini ya gharama, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kujenga daraja hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2019/2020 TARURA imepanga kufanya usanifu wa kina wa daraja hilo ili kujua gharama halisi kwa maana ya cost estimates zinazohitaji kulijenga. Namwomba Mheshimiwa Mbunge avute subira wakati Serikali inachukua hatua hizo muhimu kwa ajili ya kutatua tatizo la kukosekana kwa daraja hilo.
MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza:-

(a) Je, ni lini Serikali itaongeza Vituo vya Afya katika Kata za Jimbo la Segerea Pamoja na kupandisha hadhi Zahanati za Kinyerezi, Segerea, Kipawa na Yombo Kiwalani ili kuondoa adha kwa wananchi wa Kata 13 wanaotegemea Kituo kimoja cha Afya?

(b) Je, ni lini Kata za Minazi Mirefu, Buguruni, Kimanga na Kisukuru zitapatiwa Zahanati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuboresha huduma za afya katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, katika mwaka wa fedha 2018/2019 Serikali iliipatia Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam; iliyokuwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri. Mwezi Februari 2021, Serikali imeipatia Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa wodi tatu kwenye Hospitali ya Halmashauri na imeitenga shilingi milioni 500 katika mwaka wa fedha 2020/ 2021 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018 na 2019/2020, Serikali iliipatia Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Guluka Kwalala na upanuzi wa Kituo cha Afya Buguruni.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia mapato yake ya ndani, imetenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vitatu vya afya na shilingi bilioni 2.7 kwa ajili ya kuongeza miundombinu katika zahati tano ili ziweze kupandishwa hadhi kuwa vituo vya afya zikiwemo Zahanati za Kinyerezi na Kiwalani katika Jimbo la Segerea.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetenga shilingi milioni 250 kwa ajili ya kukamilisha maboma matano ya zahanati katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam zikiwemo Zahanati za Bonyokwa na Tabata zilizopo katika Jimbo la Segerea. Aidha, kupitia mapato ya ndani, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imetenga shilingi bilioni 2.5 kwa ajili ya kulipa fidia kwenye maeneo ambayo yatachukuliwa na Serikali kwa ajili ya ujenzi na upanuzi wa vituo vya kutolea huduma za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuimarisha miundombinu ya huduma za afya katika Jimbo la Segerea na nchini kote ili kuendelea kuboresha huduma za afya kwa wananchi. (Makofi)
MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje kutoa elimu ya utunzaji mazingira kwa wakulima wa mbogamboga ikiwemo pamoja na hatua za kuchukua ili kulinda mazingira katika Bonde la Mto Msimbazi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imebaini uharibifu wa mazingira ya Mto Msimbazi unaofanywa na wananchi wanapofanya shughuli si za kilimo tu bali pia uchimbaji wa mchanga pamoja na umwagaji maji machafu kwenye Bonde la Mto Msimbazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia kifungu cha 57(1) cha Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004, katika kuhakikisha kwamba wakulima wa mbogamboga pamoja na wadau wengine hawaharibu mazingira ya Mto Msimbazi, Ofisi ya Makamu wa Rais imeandaa programu maalum za kuelimisha na kuhamasisha wananchi juu ya matumizi ya mwongozo wa mita 60 kwa lengo la kunusuru mazingira ya vyanzo vya maji ikiwemo Mto Msimbazi.

Aidha, Ofisi ya Makamu wa Rasi kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) imeelimisha watendaji wa Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam kwa lengo la kuhamasisha wananchi wanaofanya shughuli za kimaendeleo kwenye Bonde la Mto Msimbazi kuzingatia kanuni na miongozo ya hifadhi ya mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile, Ofisi ya Makamu wa Rais kupitia mabalozi wa mazingira imeanza utekelezaji wa kampeni kabambe ya hifadhi na usafi wa mazingira ambapo suala la hifadhi ya vyanzo vya maji ni moja ya eneo la kipaumbele katika utekelezaji wa kampeni hiyo. Nakushukuru.
MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, nini mpango wa kuhakikisha Madereva wa magari ya abiria na mizigo wanapewa mikataba ya kazi ili kupata mafao na Bima za Afya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kusimamia Sheria za Kazi na kuwahimiza waajiri wote nchini kuwapatia wafanyakazi wao mikataba ya ajira kwa kuwa hili ni takwa la kisheria na ni haki ya wafanyakazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhimza hili Serikali ilitoa tamko na maagizo kwa wamiliki wa mabasi na malori tarehe 12 Juni, 2022 na tarehe 22 Julai, 2022, kwamba ifikapo tarehe 30 Agosti, 2022, wafanyakazi madereva wote wawe wamepewa mikataba kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa taarifa katika Bunge lako Tukufu kuwa waajiri wengi wametekeleza na baadhi bado wanaendelea kutekeleza mikataba hiyo kwa ajili ya kuwapatia madereva, lakini pia wafanyakazi wote katika sekta rasmi nchini. Aidha, Ofisi imejipanga na inaendelea kufanya ukaguzi maalum katika Sekta ya Usafirishaji na kuchukua hatua stahiki kwa waajiri wanao kiuka takwa hilo la kutoa mikataba kwa wafanyakazi madereva na Sekta nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kutambua na kulinda haki za wafanyakazi madereva, imeweka utaratibu wa kukaa Vikao vya Mashauriano na Majadiliano na Viongozi wa Vyama vya Wamiliki wa Vyombo vya Usafirishaji (Malori na Mabasi) pamoja na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi Madereva kwa lengo la kupeana taarifa kuhusu changamoto zinazowakabili madereva na kuzitafutia ufumbuzi. Aidha, utaratibu huu ni endelevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti mbali na kaguzi hizo, nitoe rai na kumwomba Mheshimiwa Mbunge na Watanzania wote kutoa taarifa endapo watapata taarifa za kutokuwepo kwa mwajiri katika sekta hii ambaye bado hajatekeleza maagizo haya ya Serikali kwa kutoa mikataba ya ajira kwa wafanyakazi madereva, hatua stahiki zitaendelea kuchukuliwa pia kwa mujibu wa sheria kwa kutambua kwamba sekta hii ni muhimu na ina mchango mkubwa katika uchumi wa nchi yetu. Ahsante.
MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, ni lini adha ya Walimu kukaa chini kwa kukosa Ofisi Shule za Msingi za Maendeleo, Bonyokwa na Kinyerezi JICA itatatuliwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Jimbo la Segerea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwongozo wa kuanzishwa kwa shule yoyote ni pamoja na kuwepo kwa jengo la utawala ambalo litawawezesha Walimu kuwa na chumba maalum cha kufanyia maandalizi kabla ya kufundisha (staff room).

Mheshimiwa Spika, Shule za Msingi Maendeleo, Bonyokwa, Kinyerezi JICA na Shule ya Sekondari Kimanga hazina majengo ya utawala ambayo ndio huwa na ofisi ya walimu (staff room) hivyo, baadhi ya madarasa ya ziada yamekuwa yakitumika kama ofisi wakati Serikali ikifanya utaratibu wa kujenga ofisi.

Mhesmiwa Spika, ili kutatua changamoto ya Ofisi za Walimu katika Jiji la Dar es Salaam, Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumeielekeza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya utawala katika shule hizo.
MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo kwa kuhakikisha inajenga nyumba za Walimu kama inavyofanya kwa Majeshi ya Ulinzi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya mahitaji ya Nyumba za Walimu Nchini.

Mheshimiwa Spika, ili kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo, Serikali itaendelea kupeleka fedha kwa ajili ya kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji ikiwemo ujenzi wa nyumba za walimu kulingana na upatikanaji wa fedha kupitia vyanzo mbali mbali.

Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi bilioni 37.85 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu katika shule za Sekondari na shilingi bilioni
43.63 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu katika Shule za Msingi.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya nyumba za walimu katika maeneo ambayo kunauhitaji mkubwa likiwemo na jimbo la Segerea kadri fedha zitakavyopatikana.
MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, ni Watanzania wangapi wamejitokeza na kupata fursa ya mafunzo maalum ya ujuzi yaliyotangazwa kupitia VETA kote nchini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tangu kuanza kutekeleza Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi mwaka 2016/2017, kupitia Vyuo vya VETA, Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (FDC) na Vyuo Binafsi, jumla ya vijana walioomba mafunzo ni 215,233 na waliopatiwa mafunzo ya ujuzi ni 96,894 ambapo kati yao vijana 74,578 wamepatiwa mafunzo kwa njia ya uanagenzi na vijana 22,296 wamepatiwa mafunzo kupitia njia ya urasimishaji ujuzi (RPL).

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO K.n.y. MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inawapa elimu ya utunzaji mazingira wananchi wanaofanya shughuli za kilimo katika vyanzo na njia za mito ili wafanye kilimo bila kuleta athari za mazingira?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ipo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha mpango mkakati wa kutoa elimu kwa umma wa miaka mitano na lengo la mpango mkakati huu ni kuhamasisha umma wa Tanzania kuhusu maendeleo endelevu pamoja na uhifadhi wa mazingira. Mkakati huu umehusisha namna ya utoaji elimu kuhusu matumizi ya ardhi ndani ya mita 60 katika maeneo ya vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, licha ya Serikali kuruhusu wananchi kufanya shughuli za kilimo kwa umbali wa mita 60 katika maeneo ya vyanzo vya maji, bado kuna changamoto nyingi za uharibifu mkubwa wa mazingira. Hivyo, naomba nichukue fursa hii kuwaomba viongozi wenzangu wa siasa tutumie uwezo wa kuwashawishi na kuhamasisha jamii zinazofanya shughuli za kiuchumi katika maeneo ya vyanzo vya maji na kuhifadhi mazingira.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza:-

Je, Serikali imejipangaje kushirikiana na Sekta Binafsi kuhakikisha vijana wanaohitimu wanapata ajira?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha vijana wanaohitimu wanapata ajira, Serikali kwa kushirikiana na Sekta Binafsi imejipanga kufanya yafuatayo:-

(i) Kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuwezesha Sekta Binafsi kuwekeza kwenye sekta zinazoweza kuzalisha fursa nyingi za ajira na hivyo kuwezesha vijana wengi wahitimu kupata fursa za ajira;

(ii) Kuendelea kutekeleza programu ya mafunzo ya uzoefu wa kazi (Internship) kwa vijana wahitimu wa ngazi mbalimbali za elimu na mafunzo ili kuwawezesha vijana husika kuwa na ujuzi unaohitajika na waajiri wa Sekta Binafsi wa ndani na nje ya nchi;

(iii) Serikali inaendelea kufanya majadiliano na Nchi za kimkakati kwa lengo la kuwezesha kuwa na Hati za Mashirikiano ya Uwili (Bilateral Agreements) ili kuwezesha Watanzania kunufaika na fursa za ajira zinazotokana na utangamano wa kikanda pamoja na ushirikiano wa kidiplomasia;

(iv) Serikali kupitia Wizara ya Kilimo inaendelea kutekeleza Programu ya kuwezesha vijana kushiriki katika Kilimo Biashara (Building a Better Tomorrow Youth Initiative for Agribusiness – BBTYIA);

(v) Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kutekeleza programu ya mafunzo ya vitendo (Atamizi) kwa wahitimu wa fani za uvuvi na ukuzaji viumbe maji; na

(vi) Serikali kupitia Wizara ya Madini imeendelea kuwezesha wachimbaji wadogo wa madini kwa kuwatengea maeneo pamoja na kufanya utafiti ili kuwa na uhakika wa kupata madini, kuanzisha vituo zaidi ya 93 na Ofisi za masoko 42 za kuuzia madani na hii inawapa fursa za ajira, ahsante.
MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya wananchi wa Kipunguni waliozuiwa kuendeleza maeneo yao kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Kamoli, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo katika hatua za mwisho za kufanya uthamini mpya kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi wote wa Kipunguni waliopisha ununuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA). Zoezi la uthamini linatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2022. Ahsante.