Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Mohamed Omary Mchengerwa (2 total)

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu nakushukuru sana kwa majibu mazuri ambayo ninaamini yamekidhi kiu ya Watanzania wengi wanyonge, hususan Watanzania ambao wamekuwa wakikosa maendeleo, hususan wa Jimbo langu ya Rufiji. Ninaamini sasa Sheria hii itaweza kusaidia upatikanaji wa maendeleo kwa Jimbo langu la Rufiji, hususan ujenzi wa Barabara ya Nyamwage – Utete. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ufafanuzi tu kuhusiana na hilo, labda ni kama ombi tu kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa sababu majibu ni mazuri, ni lini sasa Serikali itaamua mambo haya ya maadili yaingie katika Mitaala ya Shule za Sekondari na Shule za Msingi ili vijana wetu wawe na maadili? Msingi wa maadili uanzie Shule za Msingi na Sekondari.
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mchengerwa, Mbunge wa Rufiji, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napokea ombi lako na ni ombi zuri kwamba, ili tujenge maadili mema tunatakiwa tuanze kutoka ngazi za chini, lakini njia ambayo tumeitumia ni kwamba, watumishi wetu hawa ambao pia wameapa kuwa watumishi wenye maadili mema, wakiwemo Walimu ambao wanafanya kazi yao kwa weledi mkubwa, ndio ngazi ya awali ambayo wanasimamia vizuri vijana wetu kutoka ngazi ya shule, wanawalea watoto wetu, wanawasimamia kuwa na nidhamu, kuwa waadilifu, lakini pia, wanadhibiti vitendo vya wizi miongozi mwao ni sehemu ya mafunzo tosha ikiwa ni sehemu ya malezi ambayo yanatolewa na ngazi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutaendelea kuimarisha mabadiliko ya mitaala yetu kwa kuingiza maeneo haya ya utumishi bora, maadili mema ili tupate Watanzania wengi wenye maadili na hatimaye huko mbele tuweze kujihakikishia na shughuli zote za maendeleo nchini tukiamini kwamba kila mmoja atakuwa amelelewa vizuri kwenye familia yake anapokwenda shuleni na pia hata kwenye utumishi kufuata pia Sheria na Kanuni ili kuleta matokeo mazuri. Ahsante sana.
MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA:
Mheshimiwa Naibu Spika,
Mheshimiwa Waziri Mkuu nakushukuru sana kwa majibu mazuri ambayo ninaamini yamekidhi kiu ya Watanzania wengi wanyonge, hususan Watanzania ambao wamekuwa wakikosa maendeleo, hususan wa Jimbo langu ya Rufiji.
Ninaamini sasa Sheria hii itaweza kusaidia upatikanaji wa maendeleo kwa Jimbo langu la Rufiji, hususan ujenzi wa Barabara ya Nyamwage –
Utete.
Mheshimiwa Naibu Spika, ufafanuzi tu kuhusiana na hilo, labda ni kama ombi tu kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa sababu majibu ni mazuri, ni lini sasa Serikali itaamua mambo haya ya maadili yaingie katika Mitaala ya Shule za Sekondari na Shule za Msingi ili vijana wetu wawe na maadili? Msingi wa maadili uanzie Shule za Msingi na Sekondari.
WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza
la Mheshimiwa Mchengerwa, Mbunge wa Rufiji, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napokea ombi lako na ni ombi zuri kwamba, ili
tujenge maadili mema tunatakiwa tuanze kutoka ngazi za chini, lakini njia ambayo tumeitumia ni kwamba, watumishi wetu hawa ambao pia wameapa kuwa watumishi wenye maadili mema, wakiwemo Walimu ambao wanafanya kazi yao kwa weledi mkubwa, ndio ngazi ya awali ambayo wanasimamia vizuri vijana wetu kutoka ngazi ya shule, wanawalea watoto wetu, wanawasimamia kuwa na nidhamu, kuwa waadilifu, lakini pia, wanadhibiti vitendo vya wizi miongozi mwao ni sehemu ya mafunzo tosha ikiwa ni sehemu ya malezi ambayo yanatolewa na ngazi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutaendelea kuimarisha mabadiliko
ya mitaala yetu kwa kuingiza maeneo haya ya utumishi bora, maadili mema ili tupate Watanzania wengi wenye maadili na hatimaye huko mbele tuweze kujihakikishia na shughuli zote za maendeleo nchini tukiamini kwamba kila mmoja atakuwa amelelewa vizuri kwenye familia yake anapokwenda shuleni na pia hata kwenye utumishi kufuata pia Sheria na Kanuni ili kuleta matokeo mazuri. Ahsante sana.