Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu (26 total)

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, Kumbukumbu za Bunge (Hansard) zinaonesha kwamba swali hili liliwahi kuulizwa mara nyingi na Wizara imekuwa ikitoa maelezo tofauti tofauti ikiwapo na kusema kwamba machungwa ya Muheza siyo mazuri wakati machungwa ya Muheza sasa hivi ni mazuri, tunatumia mbegu ya Valencia, Washington na Msasa na kwamba machungwa hayo yanapelekwa Kenya na kutengeneza juice ya Del Monte. Swali langu la kwanza, Mheshimiwa Waziri atanithibitishiaje kwamba hii Kampuni ya SASUMUA HOLDING ni kweli inataka kujenga hicho kiwanda Mkoa wa Tanga? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ninao wawekezaji ambao wanataka kufanya Muheza iwe kituo cha matunda. Mheshimiwa Waziri atanithibitishia kwamba wawekezaji hao hawatapata usumbufu nitakapowaleta kwake? Nashukuru.
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, unapoulizwa swali na Mheshimiwa Mbunge ambaye amewahi kuwa Kamanda halafu ni Balozi inakuwa shida kumjibu. Nimezungumza na watu wa TAHA (Tanzania Horticultural Association) kupita Mkurugenzi Mkuu wao Jacqueline na nimezungumza na SASUMUA HOLDING, vifaa vyao kama earth equipment vimeshafika Kwamsisi, nimeviona na wamenihakikishia. Jambo la kukupa amani ya moyo Mheshimiwa Adadi ni kwamba mimi na wewe pamoja na Waziri, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba na Mheshimiwa Mboni, Mbunge wa Handeni tutapanga twende pale tuone shughuli zinazofanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tuna shughuli ya msingi kwamba yule mtu anataka outgrowers hekta 3,000 na yeye mwenyewe hekta 17,000 na anasema atawapa service. Kwa hiyo, ni jukumu lako Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote wa Tanga mkiongozwa na Mheshimiwa Mboni, mimi na Waziri mwenzangu pacha twende pale tuone Kashenamboni, tuamini au tusiamini mimi na wewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo ninalolipenda kuliko yote ni hili swali lako la pili kwamba niko tayari. Leo nina shughuli tena shughuli pevu, nakuomba kesho uniache nipumzike Jumatano walete wawekezaji wako, hakikisha Tanga hakuna vikwazo, mimi saini yangu natembea nayo.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Wakulima hawa wa Derema 1,128 wamekuwa na malalamiko ya muda mrefu na malalamiko yao hasa yanazingatia kwamba fedha ambazo wamelipwa fidia ni ndogo sana. Fedha hizo zimezingatia shina la mti wa iliki na shina la mti wa karafuu, halikuzingatia mazao ambayo yanatokana na yale mashina.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu, kwa kuzingatia ubinadamu, acha mbali hizo sheria: Je, Serikali iko tayari kuwaongezea wakulima hawa wa Derema fidia hiyo?
Pili, ni kweli kabisa kwamba wakulima hawa wanatakiwa kuhamishwa na unapomhamisha mtu inahitaji fedha nyingi sana. Wiki mbili zilizopita Waziri Lukuvi alikuwepo kwenye maeneo hayo ya Kibaranga, ametukabidhi hati ya shamba lililofutwa na Mheshimiwa Rais na tunategemea kuwahamisha watu hawa wa Derema kwenye shamba hilo la Kibaranga, lakini uwezo wa kujenga hawana. Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kuja kuongea na wananchi hawa wa Derema ili aweze kuwapa matumaini kwamba wataongezewa fidia yao kidogo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kuhusu swali la kwanza; kwanza, nampongeza kwa kuwaonea huruma wananchi wa Jimbo lake, lakini pia nampongeza kwa jitihada anazofanya kwa kuwatetea kila itakavyowezekana ili waweze kupata wanachostahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ameshasema hata yeye mwenyewe kwamba majibu haya ni kwa mujibu wa sheria na utekelezaji wa ulipaji wa fidia pale awali ni kwa mujibu wa sheria na sasa anauliza kama Serikali inaweza kuangalia upande mwingine wa ubinadamu, nafikiri hoja ya msingi pale ni kuangalia kwamba fidia ambazo zinalipwa mahali pote, kwa nchi nzima kwa kweli, ziko kwenye viwango ambavyo vinatazamwa kuwa ni vya chini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ubinadamu utatumika katika kwenda kuangalia upya sera na utatumika kwenda kuangalia upya sheria ili tuanzie kwenye ubinadamu lakini turekebishe sera zetu na sheria zetu kwa kuzingatia ubanadamu huo na ukweli na uhalisia ili malipo yaweze kulipwa kwa namna ambayo wananchi watakuwa wameona inakidhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili, nafikiri ni kama mwaliko kwamba niweze kupata nafasi ya kwenda, kwa sababu nikienda nitaona; na kuona ni kuamini. Basi namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, siyo tu mimi kwenda, nafikiri tuongozane naye twende tukaangalie, tuzungumze na wananchi hawa pengine tuwape elimu zaidi na kuweza kushirikiana nao katika kuona ukweli na kuweza kuona jambo gani linawezekana kufanyika kwa maslahi ya Taifa.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, maombi ya kuanzisha Mji huo sasa hivi ni miaka tisa, tangu mwaka 2007. Nataka Mheshimiwa Waziri anihakikishie; ni lini, wataalam wake wa kwenda kuhakiki watafika Muheza?
Swali la pili, Jimbo la Muheza linaweza kuwa ni kubwa kuliko Majimbo yote hapa mjengoni, lina kata 37, vijiji 135, vitongoji 530 unafikiria ni lini Jimbo hilo linaweza kugawiwa? Ahsante
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumbukumbu halali tulizokuwa nazo, ni kwamba kikao cha RCC kilikaa Novemba 2013; na mchakato huu maana yake ulienda kuja katika Ofisi ya Rais, lakini kipindi hicho ikiwa Ofisi ya Waziri Mkuu. Ndiyo maana hapa juzi juzi Waziri wangu mwenye dhamana, Mheshimiwa George Simbachawene, aliwaambia wataalam wetu kuleta analysis ya kila Halmashauri na kila Mkoa. Nadhani wameomba na wanaangalia iko katika status gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo haya ya Jimbo lako Mheshimiwa Adadi, ni kwamba wataalamu wetu katika kipindi hiki cha hivi sasa, bajeti wanayoshughulika nayo ni kwamba maeneo ya kipaumbele cha kwanza, itakuwa kuja kwako Muheza lakini hali kadhalika kwenda katika Mji huu wa Mombo ambapo maeneo haya maombi yao yote yameletwa pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Adadi Rajab usiwe na mashaka, hata ndugu yangu hapa Mheshimiwa Profesa Maji Marefu mambo yenu yote yakiwa yako jikoni yanaendelea kufanyiwa vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kugawanya Kata ili Jimbo la Muheza kuwa katika Majimbo mawili, naomba niseme kwamba kwa sababu jambo hili haliko kwetu, TAMISEMI, liko katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi; ambapo ikiona kama inafaa kwa vigezo, basi labda Jimbo hili linawezekana litaweza kugawa kama Majimbo mengine yalivyogawiwa.
Kwa hiyo, nina imani Tume ya Taifa ya Uchaguzi, wataangalia kufanya analysis, kuangalia ukubwa wa Jimbo hili, kwa sababu kuna Kata 37 na vijiji zaidi ya 135 wataangalia kwamba katika uchaguzi ujao, inawezekana saa nyingine wao watakavyoona inatosha, watafanya maamuzi sahihi katika eneo hilo.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, ni kweli kabisa kwamba viungo vina soko kubwa ndani na nje ya nchi kwa sababu mimi mwenyewe naona jinsi hawa wanunuzi wa kutoka nje wanavyohangaika wakati wa msimu pale Muheza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la kwanza, ni lini Wizara itawapeleka wataalam hao kuhakikisha kwamba wanainua ubora wa wakulima hao waweze kujua namna ya kulima vizuri pamoja na kuhifadhi mazao hayo ambayo wanayazagaza nje nje tu?
La pili, kama ambavyo Wizara imesema kwamba imetenga fedha za kusaidia bustani pamoja na wakulima wa hivi viungo, mna uhakika gani kwamba wakulima wangu wa Amani na Muheza fedha hizo ambazo zimetengwa watazipata?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ni lini wataalam wa Wizara wataenda kushirikiana na wakulima katika Jimbo lake ili kuweza kuwa na kilimo cha tija, nimfahamishe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba utaratibu wa kutoa taaluma na uelewa kwa wakulima ni utaratibu ambao ni endelevu kupitia Maafisa Ugani.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunajua kwamba kuna changamoto ndiyo zinawakabili, lakini katika bajeti yetu na ile ya TAMISEMI zimetengwa fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Maafisa Ugani wanafanya kazi na kuweza kuwafikia wakulima ili waweze kuzalisha kwa tija zaidi.
Vilevile labda nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sababu Pemba tuna kiwanda kizuri sana ambacho kinachakata viungo, tutashirikiana na Halmashauri ili kuona namna gani wakulima wanaweza vilevile wakaendelea kutembelea kiwanda hicho na kujifunza kinachofanyika ili pamoja na kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara, tuangalie ni namna gani tunaweza vile vile kuwa na kiwanda kinachoweza kuchakata viungo ili tufikie ufanisi kama walivyofikia wenzetu kutoka Pemba.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwamba tutafanya vipi kuhakikisha kwamba fedha zilizotengwa zinawafikia wakulima; nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ya Awamu ya Tano inatembea katika ahadi zake. Kwa hiyo, yale yote ambayo tumepanga na kutenga kwa ajili ya wakulima wetu, tutahakikisha kwamba tunafuatilia ili ziweze kuwafikia bila kupotea.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ningependa kuuliza maswali mawili. Kwanza ningependa kuipongeza Wizara hiyo kwa sababu Waziri wake Profesa Muhongo alifika kwenye baadhi ya kata za Jimbo la Muheza ambalo liko jirani na power station ya Hale na akasikiliza kilio cha Wana-Muheza kwenye Kata hizo za Kwafungo, Songa, Bwembwera na Makole. Mheshimwa Mwenyekiti, sasa swali langu la kwanza ni hili, REA Awamu ya Pili na ya Kwanza iliweka mkandarasi, na mkandarasi yule alikuwa hatimizi wajibu wake kwa wakati, kwa sababu alikuwa ana kazi nyingi sana. Sasa Serikali itawahakikishiaje wanamuheza kwamba REA hii Awamu ya Tatu itakapoanza mkandarasi ambaye atateuliwa atadhibitiwa na atafanya kazi hizo kwa wakati? (Makofi) Swali langu la pili, ni kwamba REA Awamu ya Pili na ya Kwanza ilipitisha nguzo kwenye baadhi ya vijiji na vitongoji lakini vitongoji na vijiji vile havikupata umeme. Sasa kwenye hii Awamu ya Tatu vijiji ambavyo vilipitiwa na nguzo tu bila kupata umeme, vitongoji na vijiji vile Serikali inasemaje kuhakikisha kwamba vijiji hivyo na vitongoji hivyo na vyenyewe vinapata umeme badala ya kuona nguzo tu zimepita mbele yao?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge Adadi Rajab anavyofatilia kwa kina sana kupatikana umeme katika katika Jimbo la Muheza. Nimpongeze sana tulipata orodha yako ya tarafa zako nne ikiwemo Tarafa ya Amani, Ngomeni, Bwembwera pamoja na Muheza yenyewe, kwa hiyo tunakupongeza sana. Mheshimiwa Mwenyekiti, mikakati ya kumaliza kazi kwa haraka, katika utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu tumefanya maboresho katika usimamizi. Maboresho ya kwanza ni pamoja na kuweka msimamizi yaani supervisingengineer ambaye kazi yake ni kumsimamia mkandarasi ili amalize kazi haraka, hiyo ni kazi ya kwanza. Pili, tumeweka kila ofisi ya Wilaya kwa wasimamizi wa TANESCO, tumeteua Meneja Maalum atakayesimamia miradi ya REA yaani yeye akilala, akiamka anakumbuka REA, kwa hiyo tunaamini kwamba atamaliza kazi kwa haraka. Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ambalo ni muhimu sana kwa Waheshimiwa Wabunge ni kwamba tumeweka sasa kila mkandarasi akiingia site lazima kwanza amshirikishe Mheshimiwa Mbunge, kwa hiyo mtatusaidia sana kwenye usimamizi wa jambo hili. Kwa hiyo, Mheshimiwa Adadi Rajab tuna hakika kwamba itakwenda kwa kasi. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na vitongoji, kwanza kama nilivyompongeza, tunajua vitongoji vyake 137 Mheshimiwa Mbunge Adadi Rajab vingi havijapata umeme, kama ambavyo nilikueleza, tunajua vitongoji vyetu tumeweka densification, mradi wa densification unaenda kwenye vitongoji vyote nchi nzima. Hivi sasa ninavyoongea katika Mkoa wa Tanga mkandarasi ameshaingia. Kwa hiyo, nikuhakikishie vitongoji vyako vyote ambavyo Mheshimiwa Mbunge unavifatilia sana ikiwemo Kitongoji cha Mambo leo, Mbwembeza, Msongambele, Mto wa Mbuzi, Kwambambere pamoja na kwa Mpota na Maramba vyote vitapata umeme.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, umuhimu wa ujenzi wa reli hii ya Tanga ambao utahusisha mpaka Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Mara una umuhimu ambao utaongeza mizigo sana kwenye reli hii. Tunahitaji iwe reli ya kisasa kutokana na viwanda ambavyo vinategemewa kujengwa kwenye ukanda huo ukitilia maanani kwamba Mkoa wa Tanga sasa hivi tuna viwanda vingi vya simenti na kuna kiwanda kikubwa sana ambacho kitaanza kujengwa karibuni kwa ajili ya simenti na ukitilia maanani kwamba kuna bomba la mafuta ambalo linatoka Hoima kule Uganda mpaka Bandari ya Tanga. Bandari ya Tanga imeshaanza kuboreshwa. Sasa nataka kumwuliza Mheshimiwa Waziri maswali mawili kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu la Mheshimiwa Waziri linaonekana ni lepesi na halina uzito, nataka kujua kuna mikakati gani ambayo imeshafanyika na Serikali kuweza kutafuta hizo fedha za kuanza ujenzi wa reli hiyo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, sasa hivi kuna changamoto kubwa katika Bandari ya Tanga ukitilia maanani kwamba Bandari ya Mombasa wameshajenga reli ya standard gauge ambayo inatoka Mombasa inakwenda Nairobi mpaka Kisumu na Tororo mpaka Kampala. Sasa sisi bado hatujaanza hiyo kazi; Mheshimiwa Waziri anaonaje suala la kuhusisha sekta binafsi katika utaratibu wa PPP ili tuweze kupata mwekezaji wa kujenga reli hii kwa haraka?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Balozi, Mheshimiwa Mbunge kwamba reli hii ya Tanga –Arusha – Musoma ni muhimu sana na ni lazima tuifanye kazi hii kwa haraka. Anafahamu na nampongeza tu kwa kazi kubwa ya kufuatilia shughuli hii pamoja na Wabunge wengine wa Mkoa wa Tanga, kwamba reli hii imeshaanza kufanyiwa kazi na hatua ya kwanza kuifanyia kazi ni kufanya hiyo feasibility study na detailed design. Nashukuru kazi hii imekamilika na tunatarajia tumlipe Mkandarasi tupate taarifa ili tukishapata hiyo taarifa yake tuweze kuanza sasa hatua za kutafuta fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na ushauri wake kwamba katika hatua hizi za kutafuta fedha ni pamoja na kutumia mfumo wa PPP. Tunakubali ushauri wenu, mmetushauri hilo na sisi tumekubali kwamba tutahakikisha tukishapata ile taarifa tutaanza hatua madhubuti za kufuata Sheria ya PPP ili ujenzi huo uanze haraka kwa sababu tukisema tujenge kwa hela zetu, reli zote hizi ambazo tunaenda nazo kwa sasa hatutaweza kwa muda mfupi. Kwa hiyo, nadhani ni wazo sahihi na tunashukuru sana kwa ushauri wenu, tutatumia njia hiyo ya PPP.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ili niulize swali moja la nyongeza. Matatizo ya maji salama na safi Muheza ni makubwa sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa juhudi ambazo wanafanya jinsi walivyoweza kubuni mradi wa kutoa maji Pongwe mpaka Muheza. Mradi huo upo karibu kuanza, nashukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba, ukombozi mkubwa ambao tunautegemea Wilayani Muheza ni maji yale yatakayotoka Zigi mpaka Mjini Muheza na vitongoji vyake. Sasa huu mradi upo kwenye mkopo wa Benki kutoka India wa dola milioni mia tano na ni mradi mmojawapo kati ya miradi 17 ambayo inategemewa kuanza. Sasa nataka kujua, kwa sababu wananchi wa Muheza wana shauku kubwa sana wa huu mradi. Huu mradi unaanza lini ili wananchi wa Muheza waweze kujua?Nakushukuru sana. (Makofi)
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwatoe wasiwasi Wananchi wa Muheza, ni kweli fedha imeshapatikana ya kuweza kujenga mradi mkubwa kutoka Mto Zigi kupeleka Mji wa Muheza. Taratibu ambazo tunazifanya sasa, kwanza tunakwenda kusaini mkataba wa financial agreements, wa fedha, tunasaini mkataba ule halafu tunaanza kufanya manunuzi ya kupata Mhandisi Mshauri atakayekwenda kufanya usanifu wa kina kwa ajili ya kuhakikisha kwamba maeneo yote ya Muheza pale yanapata maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili tumepanga kulifanya katika mwaka wa fedha 2017/2018. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie wananchi wa Muheza watakwenda kupata maji safi na salama.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Matatizo ya mawasiliano ya Mbulu Vijijini yanafanana sana na matatizo ambayo yapo kule katika Tarafa ya Amani Jimbo la Muheza hususan kwenye Kata za Misarai, Kwezitu, Mbomole na kwingineko. Sasa Serikali ina mpango gani kupeleka minara kwenye sehemu hizo na Tarafa hiyo ambayo kwa kweli mawasiliano ni tabu sana?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali ni kupeleka mawasiliano ya uhakika katika Tarafa ya Amani tukiunganisha kata zote ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja. Namwomba Mheshimiwa Balozi Adadi Rajab tuwasiliane ofisini ili tupitie kwa pamoja, tuone kata gani imesahaulika katika zile ambazo Serikali tayari imeziingiza katika mipango yake ya kutekeleza mawasiliano kwa wote.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati wa uzinduzi wa REA Awamu ya Tatu Mkoani Tanga, Naibu Waziri alikuja na mimi nilihudhuria. Tulipata orodha ya vijiji na Muheza tulipewa vijiji 44 kwenye REA Awamu ya Tatu. Baadaye orodha hiyo ilipunguzwa vijiji saba vikakosekana ambavyo ni Kwakopwe, Kibaoni, Magoda, Mbambara, Kitopeni, Masimbani na Msowero. Nataka kufahamu hatma ya vijiji hivyo kama vitarudishwa ili waweze kupata umeme kwa sababu wameshaanza kufanya matayarisho ya kuanza kufunga nyaya? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa wakati tunazindua katika Mkoa wa Tanga na tulifanya uzinduzi katika maeneo ambayo ameyasema na katika utafiti ikaonekana viko vijiji saba au vinane hivi ambavyo vitaingia kwenye densification stage ya pili.
Mheshimiwa Adadi Rajab vijiji saba vitaendelea kupatiwa umeme, kilichofanyika densification inaanza kwanza kwa miezi kumi na tano. Baada ya miezi kumi na tano tutaendelea na miezi mingine kumi na mitano mpaka tukapofikia hatua ya kukamilisha vitongoji vyote.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Adadi Rajab vijiji vyake saba si kwamba vimeondolewa bali vimepelekwa mbele ili baada ya miezi kumi tano na vyenyewe vitaanza kupelekewa umeme kwa utaratibu huu wa REA. Kwa hiyo, Mheshimiwa Adadi awape faraja wananchi wake wa Muheza kwamba bado watapelekewa umeme kupitia mradi huu.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, shamba la Kihuhwi ambalo
lipo Wilayani Muheza ni kweli lilikuwa linalima mpira na linaendelea kulima mpira na lilikuwa lina- supply kwenye kiwanda cha General Tyre - Arusha. Sasa hivi shamba hilo ni moja ya mashamba ambalo limeshafutiwa hati na Mheshimiwa Rais. Mheshimiwa Naibu Waziri, haoni sasa kutokana na matatizo ya Kiwanda cha General Tyre - Arusha, mikakati ifanyike kiwanda hicho kiwe na mashine za kisasa na kihamishiwe Wilayani Muheza ambapo nafasi tunaweza kutoa na kiwe karibu na malighafi?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anapendekeza kwamba tuhamishe Kiwanda cha General Tyre tupeleke Muheza. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari kuna timu inafanya kazi ya kuangalia namna bora ya kufufua Kiwanda cha General Tyre.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nimhakikishie tu kwamba nitawapelekea pendekezo la kuangalia kama inawezekana kupeleka Muheza, lakini zaidi zaidi ni vizuri vilevile kuangalia uwezekano wa kuanzisha kiwanda kipya Muheza.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza utaratibu huo ambao wa kuwauzia watu binafsi kwa makubaliano kwa asilimia 70 na huu wa asilimia 30 kwa kupeleka kwenye mnada hautumiki kabisa. Labda wanatumia asilimia 100 wanapeleka kwenye mnada. Kitendo hiki kimefanya vile viwanda vidogo vidogo Muheza pale, karibu viwanda kumi vyote vimekufa na ajira ambayo kila kiwanda kilikuwa kinachukua labda watu kutoka 100 – 150 wote kukosa kazi.
Sasa nataka kumuuuliza Mheshimiwa Waziri, kwa nini wasirudishe ule utaratibu ambao ulikuwepo wa hiyo asilimia 70 kwa makubaliano ili wale wenye viwanda vidogo vidogo ambao wanatunza ile misitu(tiki) pale waweze kupata ajira na kuendelea kupata morali ya kuanza kutunza?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ni kwa nini hata wale ambao wananunua kwa mnada ambao utakuta anakuja tajiri mmoja ananunua mitiki yote pale. Sasa ni kwa nini na yeye asilazimishwe kutengeneza kiwanda cha kukata ile mitiki pale pale Muheza kwa sababu hayo ni madaraka ambayo anayo Waziri kufuatana na regulations ambazo anazitengeneza? Nakushukuru Mheshimiwa Waziri.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba ukiuza kwa njia ya mnada wananchi wengi wanakuwa hawana uwezo wa kushinda ndiyo maana tumeweka utaratibu kwamba ni asilimia 30 ndiyo itakayouzwa kwenye mnada. Asilimia 30 itategemeana na makubaliano binafsi, maana yake tunafuata bei ile iliyokuwa na mnada, tunaangalia viwanda vyote vilivyoko katika eneo husika. Wale wote wanaohitaji wanapeleka maombi na wanapatiwa ili waweze kujijengea uwezo na kuweza kuzalisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala la pili ambalo amesema kwamba tumshauri huyu atakayekuwa ameshinda aweze kuwekeza katika eneo husika mimi nafikiri ni ushauri mzuri. Tutalifanyia kazi mara tutakapopata muda husika.Ahsante.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Tarafa ya Amani tunaitegemea sana pale Muheza kwa mambo ya uchumi, kukosekana kusikilizwa kwa redio kwenye maeneo hayo pamoja na televisheni hususan kwenye Kata za Mbomole, Zirai, Misarai, Amani kwenyewe na Kwezitu kunawafanya wananchi hao kukosa uzoefu ili kuweza kujifunza sehemu nyingine. Swali langu la kwanza ni kama ifuatavyo:-
Kufuatana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwamba katika mwaka huu wa fedha 2017/2018 zimetengwa bilioni tatu, nataka uwahakikishie wananchi wa Amani kwamba nao wako kwenye mpango huu ili waweze kupata uzoefu wa kuona televisheni yao na redio yao ya Taifa?
Swali langu la pili; utaratibu wa TBC wanapoweka minara kwenye vijiji kuwalipa fidia wananchi wa vijiji hivyo vya karibu ili kuimarisha ulinzi na pia kuhakikisha kwamba usalama wa minara hiyo inakuwepo. Kata yangu moja ya Potwe ina mnara wa TBC, lakini hawajapata fidia na ninaomba kama kwenye mpango huu wa sasa hivi, kwenye hii Tarafa ya Amani patakuwepo na mipango ya kuongeza usikivu, basi wananchi hao waweze kulipwa fidia.
Naomba uwahakikishie wananchi hao mambo hayo, nakushukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza ametaka kujua hizo shilingi bilioni tatu kama wao nao wako kwenye mpango huu wa kuimarisha usikivu. Labda tu nitoe maelezo kama tulivyosema nadhani sote tulisikia hotuba ya Mheshimiwa Waziri akisoma katika bajeti yetu ni kwamba ziko Wilaya nyingi sana ambazo hazina usikivu. Ziko Wilaya takribani 84 usikivu wake ni hafifu sana. Tulipoanza kujaribu kuboresha usikivu katika Wilaya zetu tano tulianzia kwanza kwa mwaka huu wa fedha katika Wilaya ya Geita na tulipoweka mitambo ile ya FM katika Mkoa wa Geita tumegundua kwamba katika utafiti wetu ni kwamba masafa yale usikivu uko katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Geita na maeneo mengine.
Kwa mfano; usikivu umekwenda mpaka Geita Mjini, umekwenda Bukombe, umekwenda Chato, umekwenda Kahama, kwa hiyo, ni imani yangu kwamba tunapoboresha meneo ya Longido na maeneo ya Rombo pengine usikivu unaweza ukaboreka katika maeneo mengine. Kwa hiyo, siyo rahisi sasa hivi kuamua kwamba hizi shilingi bilioni tatu tunaweza kuzipeleka wapi, tunatarajia tuone kwamba effect inaweza au usikivu huu katika maeneo haya tutakayoboresha yanaweza yakaenda mpaka maeneo gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tuna mpango mwingine wa kufufua ile mitambo ya zamani, mitambo ya AM ambayo yenyewe inakwenda mbali zaidi. Mwanzoni tulikuwa na mitambo minne tu ambapo mmoja ulikuwa Dodoma, mwingine Mwanza, mwingine Dare es Salaam na mmoja ulikuwepo Nachingwea, ambapo yote hii ilikuwa inapelekea usikivu katika nchi nzima. Kwa hiyo, tumeshakubaliana na wadau wa maendeleo kwamba watatusaidia kufufua mitambo hii, ili kusudi tuweze kuboresha usikivu katika nchi nzima. Ahsante.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nilikuwa na mambo mawili. Kwanza ni swali na pili ni ushauri.
Mheshimiwa Mwenyekii, ni kweli kabisa watalaam walikuja Muheza na walikwenda wakaangalia hiyo sehemu na Wana Muheza waliahamasika sana baada ya kuwaona watalaam hao. Hata hivyo tangu watalaam hao wamendoka nafikiri mwezi mmoja au miwli iliyopita bado hawajarudi. Sasa nilitaka kujua, ni lini watalaam hao watarudi tena na ujenzi wa hizi nyumba utaanza?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ambalo naona kama ni ushauri; ni kwamba eneo ambalo linajengwa ni eneo la Chatur sehemu ya Kibanda, Kata ya Kilulu na lina ekari 83. Sasa nyumba ambazo zimeshawekeana saini ni nyumba 20, kwa hiyo ina maana kwamba kuna eneo kubwa ambalo litabaki. Ni ushauri tu kwamba ni kwa nini sasa hivi Shirika la Nyumba lisianze marketing kushawishi wana Muheza waanze kulipia kwenye hizo nyumba ambazo zitajengwa ili eneo lote la ekari 83 liweze kutumika ipasavyo? Pamoja na hayo, ni vizuri wakati marketing hiyo inafanyika basi na watu wa benki wanakuwepo ili kuweza kutoa mikopo kwa wananchi wa Muheza. Nakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza anauliza ni lini watalaam hawa watarudi tena na ujenzi uanze kuanza. Naomba nimwambie tu kwamba tatizo ambalo limefanya wasianze mapema ni kwa sababu mpango wa matumizi ya eneo lile awali watu wa Muheza walipanga kama eneo la matumizi ya umma, kwa maana walikuwa wamekusudia kuweka stand pale. Sasa unapobadilisha kupeleka kwenye kujenga makazi inabidi mchakato wa kubadili matumizi ya eneo lile ufanyike. Kinachofanyika sasa ni kubatilisha ili litoke kwenye matumizi ya umma na liende kwenye eneo la makazi, wakikamilisha wataanza kazi hiyo.
Swali la pili, anasema marketing ianze kufanyika kwa ajili ya zile nyumba 10 ziweze kununuliwa. Napenda nimhakikishie tu Mheshimiwa Balozi Adadi kwamba tayari wanunuzi wameshaanza kujitokeza, wanachosubiri ni kuona nini kinafanyika pale. Kwa wazo lake la kusema mabenki wasogee nadhani hilo tunalichukua na ni kawaida ya National Housing wanafanyakazi sambamba na mabenki katika zoezi zima la uendelezaji miliki.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Tarafa ya Amani tunaitegemea sana pale Muheza kwa mambo ya uchumi, kukosekana kusikilizwa kwa redio kwenye maeneo hayo pamoja na televisheni hususan kwenye Kata za Mbomole, Zirai, Misarai, Amani kwenyewe na Kwezitu kunawafanya wananchi hao kukosa uzoefu ili kuweza kujifunza sehemu nyingine. Swali langu la kwanza ni kama ifuatavyo:-
Kufuatana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwamba katika mwaka huu wa fedha 2017/2018 zimetengwa bilioni tatu, nataka uwahakikishie wananchi wa Amani kwamba nao wako kwenye mpango huu ili waweze kupata uzoefu wa kuona televisheni yao na redio yao ya Taifa?
Swali langu la pili; utaratibu wa TBC wanapoweka minara kwenye vijiji kuwalipa fidia wananchi wa vijiji hivyo vya karibu ili kuimarisha ulinzi na pia kuhakikisha kwamba usalama wa minara hiyo inakuwepo. Kata yangu moja ya Potwe ina mnara wa TBC, lakini hawajapata fidia na ninaomba kama kwenye mpango huu wa sasa hivi, kwenye hii Tarafa ya Amani patakuwepo na mipango ya kuongeza usikivu, basi wananchi hao waweze kulipwa fidia.
Naomba uwahakikishie wananchi hao mambo hayo, nakushukuru. (Makofi
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza ametaka kujua hizo shilingi bilioni tatu kama wao nao wako kwenye mpango huu wa kuimarisha usikivu. Labda tu nitoe maelezo kama tulivyosema nadhani sote tulisikia hotuba ya Mheshimiwa Waziri akisoma katika bajeti yetu ni kwamba ziko Wilaya nyingi sana ambazo hazina usikivu. Ziko Wilaya takribani 84 usikivu wake ni hafifu sana. Tulipoanza kujaribu kuboresha usikivu katika Wilaya zetu tano tulianzia kwanza kwa mwaka huu wa fedha katika Wilaya ya Geita na tulipoweka mitambo ile ya FM katika Mkoa wa Geita tumegundua kwamba katika utafiti wetu ni kwamba masafa yale usikivu uko katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Geita na maeneo mengine.
Kwa mfano; usikivu umekwenda mpaka Geita Mjini, umekwenda Bukombe, umekwenda Chato, umekwenda Kahama, kwa hiyo, ni imani yangu kwamba tunapoboresha meneo ya Longido na maeneo ya Rombo pengine usikivu unaweza ukaboreka katika maeneo mengine. Kwa hiyo, siyo rahisi sasa hivi kuamua kwamba hizi shilingi bilioni tatu tunaweza kuzipeleka wapi, tunatarajia tuone kwamba effect inaweza au usikivu huu katika maeneo haya tutakayoboresha yanaweza yakaenda mpaka maeneo gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tuna mpango mwingine wa kufufua ile mitambo ya zamani, mitambo ya AM ambayo yenyewe inakwenda mbali zaidi. Mwanzoni tulikuwa na mitambo minne tu ambapo mmoja ulikuwa Dodoma, mwingine Mwanza, mwingine Dare es Salaam na mmoja ulikuwepo Nachingwea, ambapo yote hii ilikuwa inapelekea usikivu katika nchi nzima. Kwa hiyo, tumeshakubaliana na wadau wa maendeleo kwamba watatusaidia kufufua mitambo hii, ili kusudi tuweze kuboresha usikivu katika nchi nzima. Ahsante.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwanza nampongeza kwa kazi nzuri ambazo anazifanya kwa ufuatiliaji wake. Hata hivyo, zao hili la mkonge Serikali haijalipa umuhimu unaostahili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais alifuta hati za mashamba mbalimbali Mkoani Tanga na katika zile hati, Halmashauri zetu zimeshatenga maeneo maalum ya kutafuta wawekezaji. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri tushirikiane kupata wawekezaji wa kuaminika ili kuweza kuja kuwekeza kwenye hili zao la mkonge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili. La kwanza, tulikuwa tunahitaji sana Mkutano wa Wadau wa Mkonge ambao unajumuisha Wabunge ili tuweze kujadili kwa undani zao hili la mkonge na kuona namna gani tunaweza kulifufua. Sasa Wizara iko tayari kuitisha mkutano huo mapema ili tuweze kujadili suala hilo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Kampuni ya Katani Limited iliingia mkataba na wakulima wa mkonge mbalimbali katika Mkoa wa Tanga na mkataba huo umekuwa unalalamikiwa sana na wadau hawa (outgrowers) ambao wanalima mkonge. Wizara ina mpango gani, pamoja na kuboresha mkataba huo, kumilikisha wale wakulima wadogo wadogo ardhi ambazo wamepewa na Katani Limited? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Balozi Adadi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nami naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Balozi, amekuwa akifuatilia juu ya zao hili la mkonge hata pale ofisini kwangu amekuja mara kwa mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la kwanza, ni kweli tumegundua kabisa kwamba mikataba hii ya wale wakulima wadogo wa mkonge haiwanufaishi wao. Nasi kama Serikali tumejipanga kuhakikisha kwamba kabla ya mwezi huu tutaitisha kikao kikubwa sana cha wadau kwa maana ya kwamba wale wakulima wadogo (outgrowers) kupitia chama chao kile cha SISO, Bodi ya Mkonge pia Mamlaka ile ya Katani Limited pamoja na Msajili wa Hazina na Wabunge wote wa Mkoa wa Tanga ili tuweze kujadiliana na kukubaliana kwa pamoja na mwisho wa siku mkulima aweze kunufaika na tuweze kuwa na win-win situation.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali lake la pili ni kwamba sisi kama Serikali tumeshaanza kufanya ile mapping na survey katika hatua za awali na namwomba Mheshimiwa Mbunge awasiliane pia na Halmashauri. Nitoe rai kwa Halmashauri husika iwasilishe na ihakikishe inashiriki katika zoezi zima la kuwamilikisha wakulima hawa kwa njia zote ili waweze kupata haki yao. Ahsante.
MHE. ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali moja kuhusiana na bodaboda hapa nchini.
Mheshimiwa Spika, kumekuwa na mapendekezo ya kuleta mabadiliko ya baadhi ya sheria za usalama barabarani, ikiwepo bodaboda. Kwa sababu, takwimu zinaonesha kwamba vifo vinavyosababishwa na ajali barabarani bodaboda zinaongoza. Chama cha Wabunge kimetoa mapendekezo ya kuleta hapa Bungeni mabadiliko ya sheria hiyo. Ni lini Wizara au Serikali italeta mabadiliko hayo ili yaweze kufanyiwa kazi ili kupunguza hizi ajali za barabarani, hususan, bodaboda?
WAZIRI WA MAMBO NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Adadi Rajab kwa swali zuri la nyongeza na yeye ni dictionary yetu kwenye Wizara kwa sababu ana kumbukumbu nzuri ya masuala ya Wizara hii.
Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba jambo hilo analolisemea limeshapita ngazi ya Wizara na liko ngazi ya vikao vya Makatibu Wakuu na baada ya hapo litapitia Baraza na tutaleta Bungeni kwa ajili ya ukamilishwaji wa hatua hiyo anayoiomba Mheshimiwa Mbunge.
MHE. BALOZI ADADI. M.RAJABU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza: Kwanza napenda kuwapongeza sana Mawaziri wote yeye Naibu Waziri ameshafika Muheza pamoja na Waziri mwenyewe wiki iliyopita Ijumaa alikuwa Muheza na ameonesha ishara kwamba kweli Muheza inakaribia kupata maji. Isitoshe pia Mwewe katika kipindi cha Clouds TV imesema kwamba Muheza itapata maji hivi karibuni.
Mheshimiwa Spika, mradi huu wa Zigi kutoa maji kutoka Mto Zigi mpaka Mjini Muheza ni kati ya miradi 17 ambayo tunategemea kupata mkopo wa Serikali ya India ya dola milioni 500. Nataka kujua mradi huu utaanza lini?
Mheshimiwa Spika, la pili, pale Muheza Halmashauri ya Wilaya imenunua mtambo wa kuchimba visima, lakini mtambo huu tunashindwa kuutumia kikamilifu kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Kwenye bajeti hii ya wakati huu tumepangiwa zaidi ya bilioni moja na tuna mpango wa kuchimba zaidi ya visima 50, Halmashauri imekwishapitisha.
Mheshimiwa Spika, nataka Waziri awahakikishie wananchi wa Muheza kwamba Urasimu utaondolewa, tunataka kuchukua kiasi cha fedha kutoka kwenye hiyo bilioni ambayo tumepangiwa ili tuweze kutumia mtambo huu ili tuweze kuchimba visima. Nataka Mheshimiwa Waziri awahakikishie wananchi kwamba urasimu huo utaondolewa na utasaidia ku-facilitate mipango hii iweze kuendelea.
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri, lakini niwahakikishie wananchi wa Muheza wana Mbunge mfuatiliaji.
Mheshimiwa Spika, kwa kudhamiria kwa kutatua tatizo la maji kabisa katika Mji wa Muheza tumeona haja ya kuwekeza mradi mkubwa wa maji kati ya miradi ile 17 na utekelezaji wa maji inategemea na upatikanaji wa fedha. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mpaka sasa Serikali imeshasaini mkataba na ile Serikali ya India mradi wa mkopo wa milioni 500 katika kuhakikisha kwamba tunatatua tatizo la maji.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie yeye pamoja na wananchi wa Muheza wakati wowote mradi ule utaanza mara moja. Sisi kama Wizara ya Maji tutasimamia na kufuatilia fedha zile mradi uanze mara moja na kwa wakati katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili, kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo lakini tuwapongeze kwa kununua mtambo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge leo saa saba tukutane na Katibu Mkuu wa Maji ili katika kuhakikisha namna gani tunaweza tukawasaidia wananchi wa Muheza waondokane na tatizo hilo la maji katika kuhakikisha tunawaunga mkono. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri anafahamu barabara ya Muheza – Amani, kilometa 36 ambayo aliipita, imepangiwa fedha mwaka uliopita shilingi bilioni 3 kujengwa kwa kiwango cha lami na bajeti hii pia imepangiwa shilingi bilioni 5 ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ni lini barabara hii itaanza kutengenezwa kwa sababu inazidi kuharibika? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA):
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Balozi Adadi Mohamed Rajab, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilitembelea Muheza na nilipita barabara hii Mheshimiwa Mbunge anayoizungumzia na nilizungumza na wananchi kule Amani, hata kiu ya wananchi wa maeneo yale kuunganishwa na majirani zao wa Maramba na Korogwe ni kubwa. Kuna kitu ambacho kinaendelea kuhakikisha kwamba fedha hizi sasa zinakwenda ili barabara itengenezwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli maeneo haya ni hatari kwa sababu hata barabara zake tutengeneza kwa kutumia zege la saruji kwa sababu ina miteremko mikali sana. Kwa hiyo, nimhakikishie tu Mheshimiwa Balozi Adadi, kama tulivyokubaliana nitaendelea kuhakikisha wakati wowote fedha hizi zitolewe hii barabara itengenezwe kwa wakati kwa sababu sehemu ambazo zina maporomoko makubwa ni hatari sana na wakati mwingine inakuwa kikwazo wananchi kupita kabisa katika maeneo haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali inatambua hivyo, sisi kama Wizara tutahakikisha kwamba fedha ambazo zilikuwa zimetengwa mwaka wa fedha unaoisha na mwaka unaokuja zinakwenda kutibu na kuhakikisha barabara hii inatengenezwa. Kwa hiyo, nitampa mrejesho kuona hatua gani kama Wizara tunachukua kwa kadiri tunavyopata fedha kutoka Hazina tuweze kuipelekea barabara hii ili iweze kutengenezwa na ipitike kwa urahisi.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri hayaendani na hali halisi iliyopo Amani kule taasisi kwenyewe (NIMR) ambapo majengo hayo yapo. Mheshimiwa Waziri wa Afya alifika kule na aliyaona majengo yale na baada ya kuongea na wananchi aliahidi kwamba angeweza kuleta shilingi bilioni 2 kwa ajili ya kuhakikisha kwamba chuo kikuu kile kinaanza kujengwa au majengo yale yanaanza kufanyiwa ukarabati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, NIMR ya Tanzania ina sifa kubwa sana duniani kutokana na utafiti inaoufanya. Kwa sababu majengo yale yamekaa muda mrefu na kugeuka kuwa magofu, kuna mpango gani wa haraka wa kuweza kuyanusuru?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, hata kama sheria hairuhusu kuanzisha chuo kikuu lakini inaweza kubadilishwa kwani majengo yale yana facilities zote za kuanzisha hicho chuo kikuu. Kwa kuanzia ni lini mtaanza kutoa hayo mafunzo ya vyeti pamoja na diploma ili kuweza kuokoa hali ya pale ilivyo? Nakushukuru.
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Balozi Adadi Rajab, Mbunge wa Muheza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana amekuwa akifuatilia suala hili la vituo vyetu vya utafiti vya Amani pale Muheza. Niseme kwamba Mheshimiwa Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto alipita pale na hilo tunalikiri na aliahidi kwamba majengo yale yatafanyiwa ukarabati. Niendelee kusisitiza kwamba ahadi hiyo bado ipo na sisi kama Serikali tunaendelea kujipanga kutafuta fedha ili kuyafanyia ukarabati majengo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi taasisi yetu hii ya NIMR tunaendelea kuijengea uwezo. Tulipokuwa tumeianzisha mwanzoni makusudio yalikuwa ni kuelekeza nguvu zaidi katika magonjwa ya kuambukiza lakini sasa hivi kumekuwa na mabadiliko makubwa sana katika magonjwa yasiyoambukiza na tumeanza kuona tunakuwa na magonjwa haya. Kwa hiyo, tumewaelekeza NIMR vilevile kuanza kujikita katika kufanya utafiti katika magonjwa yasiyoambukizwa. Kwa hiyo, tutapokuwa tumefanya ukarabati huo tutajaribu sasa kuhakikisha kwamba pamoja na hizi tafiti ambazo tumekuwa tunazifanya katika magonjwa ya kuambukiza vilevile tunaanzisha utaratibu wa utafiti kwa magonjwa yasiyoambukiza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, Sheria ya NIMR hairuhusu sisi kuanzisha chuo kikuu lakini haituzuii kufanya kazi na baadhi ya vyuo vikuu kwa kujenga ushirikiano wa kufanya tafiti (reseach). Katika swali lake ameuliza ni lini tutaanza sasa kutoa yale mafunzo ya muda mfupi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaendelea kujipanga na katika mwaka wa fedha ujao tunatarajia kwamba tutaanza kutoa mafunzo mafupi mafupi katika kada mbalimbali za afya.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJABU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri na yenye kutia moyo ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza:-
Mheshimiwa Spika, la kwanza, tunashukuru sana kwa kutengewa fedha hizo kwa sababu majengo ya chuo hicho yako kwenye hali mbaya sana. Hata hivyo, suala la kutengewa fedha na suala la kupelekewa fedha ni vitu viwili tofauti. Ningependa kujua, fedha hizo zilizotengwa kwa ajili ya Chuo cha Mlingano zitapelekwa lini ili kazi hiyo iweze kuanza?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili linahusiana na suala la mbegu ambazo zinafanyiwa tafiti katika Chuo hicho cha Mlingano na mbegu ya zao la chai. Atakumbuka Mheshimiwa Naibu Waziri, mwanzoni mwa mwaka huu tulikwenda na wadau, Makampuni ya Chai ya Amani kwenye ofisi yake pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Chai.
Mheshimiwa Spika, suala kubwa ambalo lilitujia huko lilikuwa ni waruhusiwe kuweza ku-blend chai hiyo hapa hapa nchini, ku-pack chai hiyo hapa nchini; na badala ya kwenda kuuza kwenye mnada chai hiyo kule Mombasa. Sasa alielekeza mambo fulani fulani yafanyike na yameshafanyika na naambiwa mambo hayo yako kwenye Wizara na bado hawajayatolea uamuzi. Ni vizuri sasa hivi akaliambia Bunge hili na wananchi wa Muheza kwamba uamuzi huo ni vipi, kwa sababu tunataka kuweka kiwanda…
…kwa hiyo, nataka kujua uamuzi wa Serikali ni nini?
Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA): Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba nimpongeze sana; ni kweli alifika ofisini kwangu kuulizia swali lake la pili, juu ya kiwanda kile cha East Usangara ambapo wao wanafanya usindikaji na walikuwa wanataka kufanya blending.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake hili la (b) ni kwamba, sisi kama Serikali tulikuwa na policy mwaka 2006 kwamba wale wasindikaji wote wa chai wawe wanaomba separate registration wanapotaka kufanya blending. Katika kuepuka ukiritimba ni kwamba Bodi ya Wakurugenzi imeshakaa kuhakikisha kwamba tunawatendea haki wafanyabiashara wote na kuboresha zao la chai ili sasa yule ambaye anasindika aweze pia kupata na kufanya blending ama packaging kama anataka. Jambo hili tumeshaanza kulifanyia kazi ndani ya wiki mbili litakuwa limeshakamilika.
Mheshimiwa Spika, lakini nikija katika swali lake lile la kwanza, ni kwamba sasa hivi vyuo hivi vya kilimo ambavyo nimezungumzia, Chuo cha Mlingano chenyewe kimetengewa Sh.570,000,000 kwa sababu ile bilioni nne ni katika vyuo vyote nchini; na hizi Sh.570,000,000 mwezi ujao wa Desemba zitakuwa tayari zimeshafika ndani ya chuo.
Mheshimiwa Spika, ahsante.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ambayo sijaridhika nayo ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la Serikali la kuzuia wanyama hai kusafirishwa nje ya nchi nina hakika lilikuwa ni zuri lakini lilikuwa linalenga wanyama hai wakubwa, sidhani kama Serikali ilikuwa inalenga vipepeo ambao ni kama wadudu. Wananchi hawa wa Fanusi wamekuwa wakifanya biashara hii ya kupeleka vipepeo nje ya nchi kwa muda na walikuwa wanapata pato zuri tu, karibu shilingi laki tatu mpaka nne kwa mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi hiki ambacho Serikali imezuia biashara hii wananchi wamepata matatizo sana. Naibu Waziri mmepiga marufuku biashara hii kwa muda wa miaka mitatu ambayo inakwisha Mei mwaka huu. Je, baada ya muda huo Wizara itakuwa tayari kuwapelekea rasmi barua wanakijiji wa Fanusi ili biashara hiyo iweze kuanza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Waziri mwenyewe alifika kwenye maeneo haya na alitembea pale kwenye Kijiji cha Fanusi na kuona wananchi namna walivyobuni na kuanza huu mradi wa kufuga hawa vipepeo. Aliahidi na kumwelekeza Mkurungezi Mkuu wa TFS apeleke wataalam ili aweze kuwasaidia wale wananchi kukuza ubunifu wao na pia kuboresha mazingira yale. Ni lini wataalam hao na uboreshaji huo utaanza? Nakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Balozi Adadi Mohamed Rajab, Mbunge wa Muheza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba wakati tunazuia uuzwaji wa wanyama hawa hai nje ya nchi wapo wananchi wa vikundi mbalimbali walikuwa na vikundi vyao na walikuwa wanapata mapato na kulipa kodi kutoka na mauzo hayo. Hata hivyo, kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi ni kwamba ulitokea ukiukwaji mkubwa wa sheria na taratibu na Serikali ikaona itafute utaratibu mwingine wa kusimamia zoezi hili. Kama alivyosema itakapofika Mei, Serikali itatoa tamko sasa ni kwa namna gani tutaendelea na zoezi hili ili kutoaathiri kabisa shughuli hii hapo baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu Mheshimiwa Waziri kuagiza kupelekwa wataalam, ni imani yangu kwamba baada ya agizo la Mheshimiwa Waziri wataalam hao walielekezwa kwenda lakini kama bado hawajafika nitahakikisha kwamba wanakwenda kutoa elimu kwenye vikundi hivi ambavyo vinashughulika na biashara hii.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuongezea ziada ifuatayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilifika katika Kijiji cha Fanusi, niliona jitihada za akina mama wale katika kikundi kile na niliona adha wanayoipata kwa Serikali kuzuia kusafirisha vipepeo nje ya nchi kutokana na ile blanket ban ambayo kama Serikali tuliitoa miaka mitatu iliyopita. Naomba kuweka sawa tu rekodi kwamba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sasa hatutaruhusu tena usafirishaji wa wanyama hai kutoka nchini mwetu kwenda nchi yoyote ile na tutafanya mabadiliko ya sheria ili kuzuia jambo hilo lisitokee tena katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, utaratibu ambao tunaushauri kwa wananchi wote ambao wamekuwa wakifuga wanyamapori hawa watafute namna nyingine ya kupata faida kutokana na maliasili hiyo na siyo kutegemea kusafirisha kwenda nje ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa akina mama wa pale Fanusi niliwashauri Halmashauri na nikaagiza washirikiane na
TFS kutafuta namna ya kufanya shughuli ya utalii wa vipepeo katika eneo lile kwa sababu kwa kweli vipepeo walioko pale ni wazuri mno na watu wangeweza kwenda kuwaona pale na kingekuwa ni kivutio cha utalii na wangepata kipato ambacho walikuwa wanakitarajia. Kwa hiyo, huo ndiyo uelekeo, waondokane na mentality kwamba kuna siku tutafungulia vibali vya kusafirisha nje ya nchi kwa sababu tumezuia na hatutafungua tena.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi hii ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mji wa Muheza ni mojawapo ya sehemu ambazo zitafaidika na mradi huu kutoka India. Vile vile wakati wananchi wa Muheza wanasubiri mradi huu ambao ni mkubwa, upo mradi mwingine wa kutoa maji katika Mji wa Pongwe na kuleta Muheza Mjini. Mradi huu umefikia asilimia 70 na tumebakiza asilimia 30 tu ili wananchi wa Muheza waanze kupata maji ya uhakika. Tatizo ni uchakavu wa mabomba ambayo yako pale Mjini Muheza. Nataka kujua, ni lini Serikali itaruhusu mabomba yale yaanze kufumuliwa na kazi hiyo ianze kufanyika ili maji hayo yaweze kuunganishwa kuja Mjini Muheza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa
Mbunge, amekuwa mfuatiliaji mkubwa sana, hususan katika suala zima la utatuzi wa maji katika Jimbo lake la Muheza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Balozi Adadi ameshakutana na Mheshimiwa Waziri na tumeshakubaliana kwamba sasa ile kazi ya kuhakikisha tunaondoa yale mabomba inafanyika mara moja. Nami kama Naibu Waziri tutalisimamia katika kuhakikisha ile kazi inaanza na wananchi wake waweze kupata maji safi.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kampuni hii ya East Usambara Tea Company Limited (EUTCO)ni kampuni kubwa sana pale Muheza ambayo inalima chai na inasindika chai, sasa kampuni hii imekuwa inapeleka chai hii baada ya kuisindika kwenye mnada kule Mombasa na kule Mombasa baada ya kununua wanafanya packaging na kurudisha tena hapa nchini kuanza kuuza na hii wanaifanya kwa sababu ya kuzuiwa kupata kibali cha kuanzisha kampuni hiyo ya packaging na blending.

Mheshimiwa Spika, sasa Mheshimiwa Naibu Waziri unaweza kutoa ukaamuru sasa hivi kampuni hiyo iache kupeleka chai hiyo ambayo imesindikwa hapa nchini kwenye mnada Mombasa?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa sababu umesema, hakuna kampuni ambayo imekatazwa kufanya blending na packaging, ningependa uwaandikie barua kampuni hii ili waanze kutengeneza, waandae kiwanda cha kufanya kazi hiyo ya blending na packaging. Nakushukuru.
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza nikubaliane na mtazamo wake Mheshimiwa Balozi Adadi na nilipotembelea Muheza pia tuliweza kutembelea eneo hili na nikaona kwamba ni kweli ni kampuni kubwa ambayo inafanya kazi nzuri sana.

Mheshimiwa Spika, lakini kama ambavyo nimeeleza hapo awali, kama ni masuala ya kanuni, inabidi lazima yapitiwe na kufanyiwa marekebisho, lakini wakati huo huo, napenda pia kumsisitiza mwenye kiwanda kwamba anao uwezo wa kuanzisha hii kampuni tanzu ambayo itawezesha kuongeza thamani mpaka hatua za mwisho kupitia uzalishaji wa mashamba yake na hatua za awali ambazo anazifanya kwa sasa.

Kwa hiyo, nipende tu kuwataka wenye mashamba wote wa chai, sisi Tanzania tunahamasisha viwanda, na tungependa ajira zipatikane kupitia mlolongo mzima wa thamani katika nchi yetu. Kwa hiyo, wachukue hizo hatua lakini wakati huo tunaendelea kufanyia marekebisho ya kanuni na sheria ili kuwezesha wadau hawa kushiriki vizuri katika shughuli hii ya uongezaji thamani chai.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza ninapenda kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa sababu alifika eneo la Sakale na akazungumza na wananchi wa Sakale, na pili haikuchukua muda mrefu akawatuma hao wataalam mbalimbali ambao walikwenda wakaangalia hiyo sehemu.

Mheshimiwa Spika, tulishakubaliana na Mheshimiwa Waziri kwamba sehemu hiyo hatutaingilia eneo la Bonde la Mto Zigi ili kuepuka chanzo cha maji, na tulikubaliana kwamba tutafute wawekezaji wakubwa ambao wanaweza kuchimba eneo lile.

Mheshimiwa Spika, sasa swali langu ni, taarifa nzuri ni wawekezaji wameanza kupatikana lakini kuna tatizo la wawekezaji kuruhusiwa kuanza kuchukua sample pale na kuweza kujua kuna madini ya kiasi gani. Je, Wizara iko tayari kurahisisha utaratibu huo ili wawekezaji wale waweze kuangalia kuna madini ya kiasi gani pale Sakale?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili ni la ujumla tu la kutaka kujua. kwamba mpaka sasa hivi Wizara ina utaalam gani ambao unaweza kujua mgodi fulani kuna madini ya kiasi gani pale, kama ni dhahabu au almasi; je, utaalam huo tunao au bado hatuna?

Mheshimiwa Spika, ni hayo tu, ahsante sana.
WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Balozi Adadi Rajab kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza kwa moyo wa dhati kabisa ninaomba nikiri kwamba Mheshimiwa Balozi Adadi kwa watu wa Muheza na kwenye hilo eneo alilolitaja la uchimbaji, yeye amekuwa champion mkubwa wa kuhakikisha kwamba uchimbaji unaanza kwenye kazi hiyo kwa sababu wananchi wa pale kwa kweli ukienda wanategemea sana hilo eneo ili waweze kuchimba na kujipatia mapato na kubadilisha maisha yao.

Mheshimiwa Spika, changamoto iliyokuepo ni kwamba eneo hilo haliwezi kuchimbwa kwa uchimbaji mdogo kwa maana ya matumizi ya mercury ambayo yanaweza kingie kwenye Mto Zigi na kuathiri chanzo cha maji ambacho kwa kweli katika Bwawa la Mbayani ambalo linapeleka maji kule Tanga Mjini, Korogwe pamoja na Muheza, ukiruhusu hiyo watu wote wale maji yale yataweza kuchafuliwa na mazingira. Uchimbaji ambao unaweza kuruhusiwa pale ni ule tu uchimbaji wa kati ambao unakuwa na EIA ambayo NEMC wataitoa.

Mheshimiwa Spika, sasa kama kuna wataalam ama kuna watu wanaotaka kuchukua sampuli, hakuna mahali popote wanazuia, kwa mujibu wa sheria wanaweza kuchukua sampuli na kupima na kuweza kujua kuna madini kiasi gani. Kwanza ni jambo la faida kwetu kwa sababu wanafanya utafiti kwa niaba ya Serikali na hivyo wanaweza kuchukua wakati wowote. Kama kuna mtu yeyote anawazuia kuchukua sampuli naomba nitoe wito wafuate taratibu zote zilizowekwa wachukue sampuli waweze kwenda kupima na hatimaye wapate taarifa wanazozihitaji.

Mheshimiwa Spika, swali la pili ni je, Wizara tuna utaalam wa kujua kuna kiasi gani cha madini mahali fulani? Naomba nijibu tu kwa kifupi kwamba Serikali inayo huo uwezo kupitia Shirika letu la Serikali la GST, tuna uwezo wa kutambua kuna kiasi gani cha mashapo na kuna kiasi gani cha madini kinachoweza kuchimbwa. Kama kuna eneo ambalo analo, kwa kutumia Shirika letu la STAMICO, nimuombe Mheshimiwa Mbunge awasiliane na STAMICO waweze kujua ni kitu gani kinaweza kufanyika.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Zao la pilipili manga na viungo vingine kama hiliki na mdalasini ni mazao ambayo tunayategemea sana katika Wilaya ya Muheza, lakini wakati wa msimu wa mazao haya ya viungo panakuwa na vurugu kubwa sana Muheza hususan ya wanunuzi wa mazao haya kiasi kwamba inaelekea kushusha bei sana za viungo hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango gani kuweza kuwasaidia Wana-Muheza ili kuhakikisha kwamba inaweka maghala na kuingia kwenye utaratibu wa uuzaji wa viungo hivi kwa njia ya mnada? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; pamoja na zao hili, lakini hakuna utaratibu wa ku-add value kwenye mazao haya ya viungo; nilitaka kujua Serikali ina mpango gani wa kujaribu kuwasaidia Wana-Muheza kwa ajili ya kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya kuchakata viungo hivi ili kuviongezea thamani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. HUSSEIN M. BASHE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mpango wa Wizara ya Kilimo sasa hivi kuhakikisha kwamba tunabadilisha mfumo wa uuzaji na wanamasoko wa mazao ya kilimo kwa ujumla wake. Moja ya mkakati tulionao kama Wizara ni kuhakikisha tunafanya mfumo wa kuweko maghala na kuleta minada katika maeneo mbalimbali na mkakati huu utahusisha siyo tu mazao ya pilipili manga kama ambayo amesema Mheshimiwa Adadi, lakini vilevile tutaangalia mfumo wa uuzaji wa mazao yote hata haya tunayoita ya mkakati ikiwemo pamba kama ambavyo tumeanza kwenye chai kuhakikisha kwamba tunaanzisha soko katika Jiji la Dar es Salaam la kuuzia chai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutatuma wataalam kuangalia mambo mawili; moja, viability ya kuanzisha mfumo wa stakabadhi ghalani katika eneo la Muheza kama halitoathiri bei iliyoko sasa hivi. Kwa sababu tunaweza kwenda kuanzisha mfumo ambao ukapelekea kuangusha bei ya zao. Kama uuzaji wa kutumia stakabadhi ghalani utamwongezea mkulima bei nzuri, tutaufanya huo na tutatuma wataalam waende wakafanye tathmini ili tuweze kuanzisha Warehouse System Receipt kwa eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu value addition, nitumie nafasi hii nimwombe Mheshimiwa Mbunge wa Muhesza, kama anaweza kuwaweka wakulima wake katika makundi na uzalishaji wao ukawekwa katika makundi ya pamoja na kutengeneza vyama vya wakulima wadogo wadogo wa pilipili manga na mazao mengine katika eneo hilo, Serikali iko tayari kuwashika mkono kupitia njia mbalimbali za kuweza kuwapatia funding ili waweze kuanzisha process ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine, katika Halmashauri zetu tunakusanya fedha za cess ni lazima tutengeneze mipango ya kutumia fedha zinazotokana na mazao ya kilimo ziweze kurudi kuongeza thamani na kuwasaidia wakulima kufaidika na kodi zinazokusanywa na mazao haya ili angali zile 10% za Halmashauri, basi tuweze kuwakopesha wakulima wadogo wadogo waweze kuanzisha small process industry na pale ambapo wanahitaji msaada wa Serikali Kuu, sisi kama Wizara ya Kilimo tuko tayari kuwashika mkono. (Makofi)
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusu suala hili, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, namshukuru sana Waziri wa Madini, Mheshimiwa Doto ambaye alifika kabisa Sakale kwenye kijiji hiki na kujionea hali halisi ya pale na pili, nawashukuru sana Wizara ya Madini pamoja Mazingira, kwa kuweza kupeleka wataalam kwa haraka sana kwenda kuangalia mazingira ya eneo lile na nawashukuru sana wananchi wa Sakale na Mbomole kwa nidhamu ambayo wanaionesha kuweza kutunza chazo cha maji cha Mto Zigi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa swali langu la kwanza, ni ukweli kwamba pale dhahabu ipo kwenye Milima ya Sakale ambayo ipo karibu na Mto Zigi na dhahabu ambayo ipo pale ni ya kiwango cha juu. Sasa dhahabu ipo ndani ya mto na kwenye Milima ya Sakale. Sasa Serikali itakubaliana na mimi kwamba kuna umuhimu wa kutuma wataalam wa juu waliobobea kuweza kwenda kuangalia tena namna gani dhahabu ile inaweza kuchimbwa kutoka kwenye milima ambayo iko karibu na Mto Zigi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili ni kwamba kila wananchi wa Sakale, Mbomole wakitembea kwenye ardhi ile, wanahisia wanakanyaga dhahabu sasa na wanasikitika kwamba wanakanyaga mali ambayo ipo chini ya ardhi lakini Serikali haioni umuhimu wa kuwasaidia kutoa ile mali pale nje.

Sasa Serikali inaona umuhimu gani wa kuchukua hatua za haraka kupeleka wale wataalam na kuhakikisha kwamba wananchi wa Sakale, Mbomole na Muheza wanafaidika na dhahabu hiyo ambayo iko kwenye Milima ya Sakale? Nakushukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika milima hiyo kuna dhahabu nyingi na milima hiyo kwenda hadi kwenye Mto Zigi kuna dhahabu nyingi tu ya kutosha, lakini kwa uchimbaji mdogo kwa sababu wachimbaji wadogo wanatumia kemikali ya zebaki ambayo ni hatari sana kwa afya ya binadamu, Wizara pamoja na wataalam wameshauri kwamba uchimbaji mdogo usifanyike pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa uchimbaji wa kati na uchimbaji mkubwa hilo linawezekana, lakini cha msingi tu ni kwamba ni lazima tupate mwekezaji ambaye anaweza akafanya utafiti wa kina kuweza kujua mashapo yamekaa vipi katika milima hiyo hadi kwenye mto na vilevile aweze kuchimba na uchimbaji wa maeneo hayo inabidi uchimbe katika style ya underground badala ya open cast mining. Ni kwamba wachimbe kwa kwenda chini na wahakikishe kwamba uchimbaji ule hautaathiri vyanzo vya maji kwa sababu vyanzo vya maji vya Mto Zigi vinategemewa katika Jiji la Tanga, Wilaya ya Korogwe na Wilaya ya Muheza yenyewe. Kwa hiyo, vyanzo hivi ni muhimu sana, ukiweka uchimbaji pale, ukawa unatiririsha kemikali kwenye vyanzo vya maji, ni hatari kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama uchimbaji wa kati au wa hali ya juu kwa sababu wale wanaweza wakachimba kwenda underground na vilevile ile processing plant inabidi iwekwe mbali na eneo hilo. Kwa hiyo, kusafirisha zile rocks za dhahabu kupeleka maeneo ambayo ni ya processing plant inabidi iwe ni distance kubwa, kwa hiyo, ni lazima uwekezaji uwe ni wa hali ya juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimshauri Mheshimiwa Mbunge tuendelee kuwasiliana, tutafute wawekezaji ambao wanaweza wakafanya detailed exploration kwa maana ya kujua mashapo yamekaa vipi na wakaweza kuja na plan nzuri ya uchimbaji ambao hautaathiri mazingira, vyanzo vya maji, hilo linawezekana. Kwa hiyo, tushirikiane tu na Mheshimiwa Mbunge kwa hilo nadhani tunaweza tukafikia pazuri. Ahsante sana. (Makofi)